Showing posts with label kazi. Show all posts
Showing posts with label kazi. Show all posts

February 28, 2018

NAFASI ZA KAZI MAMLAKA YA BARABARA VIJIJINI "TARURA" MKOA WA RUVUMA

 
 

January 19, 2018

HAPO NI ENEO LA LWIKA KATIKA KIJIJI CHA LUNDO

Leo hii hakuna Mawasiliano ya Barabara toka Mbamba Bay to Kilosa....Bus zilizotoka   Mbinga na Songea Zimeishia shell pale Tambachi Kuna Calvart Limekwenda na maji watu wanahangaika hawajui cha kufanya.Hali ya mawasiliano kwa njia barabara ilikuwa mbaya sana siku ya tarehe 18/1/2017.

January 18, 2018

HAKUNA CHAMA KINACHOENDESHA MAISHA YA MPIGA KURA.

NA HONORIUS MPANGALA, BAHI
NILIPOKUWA mdogo niliamini maisha ni jambo ambalo liko tofauti na la kuogofya sana katika jamii. Sababu kubwa ni pale nilipokuwa nayasikia maneno kama “Usicheze na maisha”. Fikra zangu zilinipeleka kuwa maisha ni jitu linalotisha sana katika jamii.

Baada ya makuzi nikapata misemo kama “Maisha yenyewe ndiyo haya haya” nikaanza kutambua kumbe mwenendo wa kuanzia asubuhi unaamka hadi usiku unaingia kulala hizi harakati zote ufanyazo ndiyo maisha yenyewe.

Katika vipindi ambavyo wapiga kura na wananchi wa kawaida toka vyama vya siasa wanajiona kama na wao ni wenyechama basi ni katika kampeni za uchaguzi. Kipindi hiki kila mwanachama anajiita ni mwenyechama. Ni kipindi ambacho watu hao hudiriki kunukuu maneno ya wagombea wao na kuiaminisha hadhira aliyonayo kuwa chama chetu kitatekeleza mambo kadha wa kadha.

December 28, 2017

NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA NYASA

 Halmashauri ya wilaya ya Nyasa imetangaza nafasi za Kazi. Kwa vijana wenye sifa za kazi hiyo wanashauriwa kuomba kazi hizo mara moja. Bila kujali ni mwenyeji wa wapi, lakini sifa kubwa ni  raia wa Tanzania. Waweza kutazama kwa kufungua hapo chini...

BONYEZA HAPA KUONA TANGAZO ZIMA LA KAZI

UMENG’ATWA NA MANYIGU, LAKINI KIU BADO UNAYO.

NIKIWA njiani kurejea Dar es salaam, mdogo wangu Honorius Mpangala alinitumia ujumbe mfupi katika simu yangu, “Aisee tupo Tingitingi, lakini nimeng’atwa na manyigu. Vifaa tulibeba kama kawaida,”. 
  
Nikashangaa. Sikufikiria kama eneo lile laweza kuwa na manyigu au hatari zozote za wanyama wakali. Leo pichani anasema, “Nikiwa najikagua mkono na miguu baada ya kung'atwa na manyigu saba. Ilikuwa tarehe 25/12 saa saba mchana pori moja kando ya ziwa Nyasa.Pori lenye msitu unaogota katika maji ukiwa na mawe makubwa huko ndo maskani ya wanyama kama ngedere, nyoka, nungunungu, mijusi wa rangi rangi,ndege kama kanga pori na Kwale. Baada ya shambulizi nilijiziba uso na kuacha sehemu ya miguu kuwa wazi lakini ajabu niling'atwa hadi kwenye makalio,”.

December 27, 2017

NYASA; DISEMBA 20 ILIPONIREJESHA MIAKA 13 ILIYOPITA

NA HONORIUS MPANGALA, LUNDU
TULIANZA safari yetu na dadangu kijijini kwetu Lundu na kuelekea Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa Mbamba Bay. Changamoto za barabarani hazikukosa kwasababu ya mvua zinazonyesha. Tukifika na kukamilisha yaliyotupeleka huko. 

Saa kumi jioni nilipofika kituo cha mabasi cha Mbamba Bay sikukuta gari ya kugeuza kwenda kwetu Lundu. Ikatulazimu tupande ya kuishi njiani, gari iliyotoka Mbinga kwenda Kihagara. Nikiwa nawaza namna ya kutoka Kihagara hadi Lundu lakini nikapanga jambo kuwa bodaboda ziko kila eneo sikuhizi,na sikutoa nauli ya yangu na Dada nikamwambia waambie natoa Mimi. Nikamwambia konda natoa Kihagara kuna mtu anatusubiri,nilifanya Kwa maksudi.

November 15, 2017

MANISPAA YA SONGEA KUNUNUA MAHINDI TANI 400

NA MWANDISHI WETU, SONGEA
 
HALMASHAURI ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma imepangiwa na Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula(NFRA) katika msimu huu kununua mahindi tani 400.
Picha kwa Hisani ya Manispaa ya Songea.
Afisa Kilimo wa Manispaa ya Songea Mushoborozi Christian amesema Halmashauri hiyo imepokea barua toka NFRA inayotoa maelekezo ya ununuzi wa mahindi katika awamu ya tatu msimu wa mwaka 2017/2018.

November 13, 2017

KWANINI SEKRETARIETI YA AJIRA HAINA MATAWI NCHINI?

NA MARKUS MPANGALA
MIAKA kadhaa iliyopita nilishindwa kuwaelewa kabisa watendaji wa Wakala  wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) hapa nchini. Nilikuwa siwaelewi kwa sababu siku moja niliwahushudia wafanyabiashara fulani kutoka Songea mkoani Ruvuma, wakizunguka vyumba vya ofisi vya taasisi hiyo kwenye jengo la Ushirika liliko Barabara ya Lumumba, Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam kwa madhumuni ya kusajili kampuni yao.  
Jenista Mhagama

Pili,niliwahi kumsaidia rafiki yangu, Albert Nyaluke Sanga, ambaye ni mfanyabiashara mkubwa mkoani Iringa, ili apate leseni ya biashara. Haikuwa leseni yake binafsi, bali aliamua kumsaidia kijana mmoja aliyekuwa na ndoto za kuwa mfanyabiashara, lakini alikosa pa kunzia.
Rafiki yangu huyo anapenda kuwasaidia vijana wanaojishughulisha na ujasiriamali kwa sababu anaamini hiyo ndiyo njia pekee ya kuwakomboa, badala ya elimu yao na kuondokana na matembezi ya kusambaza bahasha za kuomba nafasi za kazi.

November 10, 2017

SOKA LA WACHINA, LIKABORESHWA UINGEREZA

NA.HONORIUS MPANGALA

INASADIKIKA Polisi wa China walikuwa wanacheza mchezo uliitwa 'Tsh-u' ikiwa na maana ya piga mpira. Mchezo huo ulipenyeza Japan na maeneo mengine ya Roma. 

Soka lilingia Uingereza mwaka 1066 wakati wa utawala wa Mfalme William. Kutokana na wachezajj wengi kupata matatizo ya vifo mfalme Edward na wengine kama Richard walipiga marufuku na kutoka kauli ambayo Kwa yoyote atakayehusika au kuonekana anacheza soka atenda jela.

November 08, 2017

WAAMUZI WETU NA MITIHANI YA SIMBA NA YANGA



NA HONORIUS MPANGALA

TANZANIA ni miongoni mwa nchi zinazotajwa kuwa na amani na hii ni kutokana na muingiliano wa mambo manne.  Yako makundi yaliyojikita katika masuala ya dini, siasa, ushabiki wa soka na mwisho hali ya kuoleana.

Kupitia makundi hayo manne kunapelekea jamii ya watanzania kuishi pamoja. Makundi hayo hukutanisha watu tofauti kutokana na ufuasi wake. Haitakuwa ajabu unapomuona Waziri wa Mambo ya Ndani na kada wa CCM Mwigulu Nchemba akikaa jukwaa moja na kiongozi wa upinzani Freeman Mbowe na kuipa hamasa klabu wanayoipenda ya Yanga. Pia haitashangaza kwa kiongozi mkuu wa chama cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe kukaa pamoja na Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa na kuipa hamasa klabu yao pendwa ya Simba. Hayo yote hufanyika bila kujali itikadi za kisiasa walizonazo.

November 02, 2017

KAMPUNI YA MKUKI NA NYOTA WAINGIA SOKO LA VITABU CHINA


NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM

KAMPUNI ya Mkuki na Nyota ambayo hujishughulisha na uchapaji wa vitabu imetanua wigo wa soko lake la uchapishaji na utangazaji wa vitabu baada ya kusaini makubaliano na Shirika la World Affairs Press (WAP) la nchini China.
 
Akizungumza baada ya kusaini makubaliano hayo Mkurugenzi wa MNN, Mkuki Bgoya amesema kuwa wamesaini Makubaliano na Shirika la World Affairs Press (WAP) ya China kufanya kazi pamoja katika miradi mbalimbali ya kuchapisha na kuvitangaza vitabu ikiwa ni njia mojawapo ya kutanua soko la kampuni hiyo barani Asia.

Mkuki na Nyota ni kampuni mashuhuri kwa uchapaji wa vitabu ambayo ilianzishwa mwaka 1992 jijini Dar es salaam. Mwanzilishi wa kampuni hiyo ni Walter Bgoya ambaye alitumia uzoefu wake wa miaka 18 ya kuwa Meneja Mkuu wa Tanzania Publishing House. 

September 30, 2014

NAFASI ZA KAZI WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

MWISHO WA KUTUMA MAOMBI NI BAADA YA SIKU 14.
*JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA*
*WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI*
*TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI*
*2. KONSTEBO WA UHAMIAJI Nafasi 114 - (Nafasi 100 kwa ajili ya* *Tanzania Bara na Zanzibar na nafasi 14 maalum kwa ajili ya Zanzibar tu)*
A. SIFA ZA MWOMBAJI:
(i) Awe Raia wa Tanzania mwenye umri kuanzia miaka 20 hadi 25.
(ii) Awe amehitimu kidato cha nne na kufaulu masomo ya Kiingereza,
Kiswahili, Historia, Jiografia, Kifaransa, Hisabati ambapo masomo matatu
kati ya hayo yawe katika kiwango cha Credit
(iii) Awe pia na mojawapo ya sifa zifuatazo:
Cheti cha Sheria;
Cheti cha Utunzaji Kumbukumbu;
Cheti cha Kompyuta;
Cheti cha Ufundi (FTC);
Cheti cha Mafunzo ya Ufundi Stadi kwenye fani ya (umeme, mitambo, bomba);
(iv) Waombaji wenye ujuzi wa mojawapo ya lugha zifuatazo (Kifaransa,
Kichina, Kijerumani, Kiarabu au Kihispania) watafikiriwa kwanza.
(v) Aidha, Mwombaji aliyepitia mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa atapewa
kipaumbele.
B. MAJUKUMU NA KAZI ZA KUFANYA
(i) Kupanga majalada ya watumiaji wa huduma za uhamiaji;
(ii) Kufungua na kutunza majalada yenye orodha ya majina ya watumiaji wa
huduma za uhamiaji;
(iii) Kufanya doria sehemu za mipakani, bandarini, vituo vya mabasi,
treni na sehemu zenye vipenyo vya kuingia na kutoka nchini;
(iv) Kukamata watuhumiwa wa makosa mbalimbali ya uhamiaji na kuwafikisha
kwenye mamlaka husika;
(v) Kufanya ukaguzi kwenye hoteli, nyumba za kulala wageni na sehemu za
biashara;
(vi) Kusindikiza watuhumiwa wa kesi za uhamiaji mahakamani pamoja na
wageni wanaofukuzwa nchini (Deportees)
(vii) Kufanya matengenezo/ukarabati wa mitambo na vitendea kazi vya
uhamiaji;
(viii) Kuandaa hati mbalimbali za uhamiaji.
3. UWASILISHAJI WA MAOMBI
Barua za maombi zinapaswa kuandikwa kwa mkono na kuwasilishwa kwa njia
ya posta zikiwa zimeambatishwa na:-
(i) Nakala ya cheti cha kuzaliwa;
(ii) Nakala ya cheti cha kuhitimu masomo ya sekondari pamoja na vyeti
kwa mujibu wa sifa nyingine zilizoainishwa kwenye kipengele A(iii).
(result slips hazitakubalika)
(iii) Nakala ya vyeti vya kumaliza shule ya msingi na sekondari (Leaving
Certificates);
(iv) Picha mbili (Passport Size);
(v) Barua ya Utambulisho kutoka kwa Mwenyekiti wa Serikali za
Mitaa/Shehia/ Vijiji;
(vi) Nakala za vyeti vyote vitakavyowasilishwa viwe vimethibitishwa na
Wakili/ Kamishna wa Viapo.
4. ANUANI YA KUWASILISHA MAOMBI
Barua za maombi ya kazi ziwasilishwe kwa njia ya posta ndani ya kipindi
cha siku 14 kuanzia tarehe ya tangazo hili kwa anuani zifuatazo:-
Waombaji wa nafasi 200 (100 Koplo na 100 Konstebo) ambazo ni kwa ajili
ya Tanzania Bara na Zanzibar wawasilishe maombi yao
kwa anuani ifuatayo:
Katibu Mkuu,
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,
S.L.P 9223,
DAR ES SALAAM.
Waombaji wa nafasi 28 (14 Koplo na 14 Konstebo) ambazo ni maalum kwa
Zanzibar wawasilishe maombi yao kwa anuani ifuatayo: Katibu Mkuu,Wizara
ya Mambo ya Ndani ya Nchi,
C/O Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar,
S.L.P 1354,
ZANZIBAR.
Maombi ambayo hayatazingatia maelekezo tajwa hapo juu hayatashughulikiwa.
CHANZO: DAILY NEWS LA TAREHE 29 SEPTEMBA 2014

May 31, 2013

NAFASI YA KAZI- GRAPHIC DESIGNER



Hi There

I am looking for a Graphic Designer
         Experience not neccesary
         Education B.A or Diploma in Graphic Arts
         Software knowledge: Photoshop, Illustrator, In Design
         Video Editing and 3D knowledge an added advantage

Please Inbox me your CV and contacts for more details
Regards

Paul Konyango

pkonyango1@gmail.com

May 29, 2013

NAFASI ZA KAZI JESHI LA POLISI NCHINI

Fuata maelekezo kadiri tangazo linavyojieleza.

April 22, 2013

NAFASI YA KAZI AFISA MAENDELEO DARAJA II


COMMUNITY DEVELOPMENT OFFICER GRADE II) – NAFASI 22
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Waajiri wafuatao:- Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, Mtwara, Sumbawanga, Simanjiro, Halmashauri ya Mji Njombe, Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba, Newala, Nkasi, Bukoba, Sengerema, Rufiji, na Mpanda na Halmashauri ya Jiji la Mwanza.
71.1 MAJUKUMU YA KAZI
Maafisa Maendeleo ya Jamii Dalaja la II watapangiwa kazi katika ngazi za Kata au Makao Makuu ya Halmashauri na kazi zao zitakuwa zifuatazo:
· Kuandaa na kupendekeza mipango na mikakakti ya kubadili fikra za watu ili waweze kuwa na mawazo ya maendeleo sawia na Sera za Serikali na wakati uliopo
· Kupitia mbinu shirikishi kuwezesha jamii kuanzisha miradi ya kijamii kama vile:-
- Usafi wa mazingira
- Ujenzi wa nyumba bora
- Ujenzi wa shule
- Ujenzi wa zahanati
- Kuchimba au kuzifanyia matengenezo barabara hasa za vijijini
- Ujenzi wa majosho
- Uchimbaji wa visima vifupi
44
- Utengenezaji wa malambo
· Kuhamasisha matumizi endelevu ya mazingira
· Kusambaza na kuhamsisha matumizi ya teknolojia sahihi kama vile uvunaji wa maji ya mvua, majiko sanifu, matumizi ya mikokoteni
· Kuhamasisha watu kutumia huduma za mafunzo ya Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi
· Kuwasadia wanachi vivijini kuandaa maandiko (Project Write ups) ya kuombea fedha za kuendesha miradi yao
· Kuhamasisha, kuandaa na kutoa elimu kwa umma kuhusu uraia na Utawala bora
· Kukusanya, kutunza, kutafsiri na kusambaza takwimu na kumbukumbu muhimu kwa ajili ya matumizi ya jamii
· Kuwezesha wananchi kupambana na mila zenye madhara kwa afya za wanchi hasa wanawake na watoto wa kike, kuenea kwa virus vya UKIMWI na magonjwa ya mlipuko.
· Kuelimisha viongozi wa Serikali za Vijiji, Dini na Mashirika yasiyo ya Kiserikali kuhusu Sera mbalimbali za Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto na kutumia Sera hizo
· Kutoa taarifa za hali ya jamii kwa ngazi mbalimbali
71.2 SIFA ZA MWOMBAJI
· Kuajiriwa wahitimu wa Shahada au Stashahada ya Juu ya Maendeleo ya Jamii kutoka Vyuo vinavyotambuliwa na Serikali katika fani zifuatazo:-
 Maendeleo ya Jamii (Community Development)
 Elimu ya Jamii (Sociology)
 Masomo ya Maendeleo (Development Studies)
 Mipango na Usimamizi wa Miradi (Project Planning and Management)
 Maendeleo na Jinsia (Gender and Development)
71.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS D kwa mwezi.
72.0 MLEZI WA WATOTO MSAIDIZI (CHILD CARE ASSISTANT) – NAFASI 5
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Manispaa ya Singida na Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga.
72.1 MAJUKUMU YA KAZI
· Kulea watoto katika vituo vya kulelea Watoto wadogo mchana
· Kutoa mafunzo kwa akina mama juu ya malezi bora ya watoto wadogo wenye umri kati ya miaka 0 hadi 8
· Kusaidia shughuli za kinga za magonjwa ya watoto vijijini/sehemu au eneo la kituo
· Kuwa kiongozi wa kituo cha malezi ya awali ya Watoto wadogo
45
72.2 SIFA ZA MWOMBAJI
· Kuajriwa wahitimu wa kidato cha nne waliofaulu mafunzo ya mwaka mmoja ya malezi ya awali ya watoto wadogo wenye umri kati ya miaka 0 hadi 8 kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali au wenye cheti cha mwaka mmoja cha mafunzo ya Ustawi wa Jamii.
72.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS B kwa mwezi.
62.0 MAENDELEO YA JAMII MSAIDIZI II (COMMUNITY DEVELOPMENT ASSISTANT GRADE II) – NAFASI 52
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Manispaa ya Mtwara na Kigoma/Ujiji. Halmashauri ya Wilaya ya Handeni, Babati, Pangani, Mkinga, Sengerema, Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Halmashauri ya Mji Njombe, Halmashauri ya Wilaya ya Rufiji, Kibondo na Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
62.1 MAJUKUMU YA KAZI
· Kuwa kiungo kati ya wanakijiji, Afisa Mtendaji wa kata na watumishi wengine wa Serikali katika kutekeleza shughuli za maendeleo
· Kuhamasisha wanakijiji katika kazi za kujitegemea
· Kubainisha na kuratibu matumizi ya rasilimali kwa miradi ya kijiji
· Kukusanya, kutunza, kutafsiri na kusaidia wanakijiji kutumia takwimu na kumbukumbu mbalimbali kwa shughuli za maendeleo ya kijiji
· Kutoa taarifa za utekelezaji wa shughuli za maendeleo kila mwezi kwa uongozi wa kijiji na kwa Afisa Maendeleo ya Jamii ngazi ya Kata
· Kuwahamisha na kuwawezesha wananchi kulinda na kuhifadhi vyanzo vya maji
37
· Kusaidia kuunda vikundi vya kijamii na kimaendeleo
· Kuratibu shughli za Asasi zisizo za kiserikali na kijamii
· Kuandaa tararifa za utekelezaji kazi vijinjini za kila mwezi, robo, nusu na mwaka mzima
· Kuratibu shughuli za kupambana na UKIMWI
62.2 SIFA ZA MWOMBAJI
· Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha IV/VI wenye Stashahada ya Maendeleo ya Jamii kutoka katika Vyuo vya Maendeleo ya Jamii (Buhare au Rungemba) au Vyuo vingine vinavyotambuliwa na Serikali.
62.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGS.C kwa mwezi
63.0 AFISA MTENDAJI WA KATA DARAJA LA II (WARD EXECUTIVE OFFICER GRADE II) – NAFASI 106
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma, Morogoro, Mtwara, Halmashauri ya Wilaya ya Babati, Bunda, Mafia, Biharamulo, Newala, Kondoa, Masasi, Mtwara na Halmashauri ya Jiji la Mwanza.
63.1 MAJUKUMU YA KAZI
· Atakuwa Mtendaji Mkuu wa Kata na kiungo cha Uongozi kwa Idara zote katika kata na atashughulikia masuala yote ya kata
· Atakuwa Mhamasishaji mkuu wa Umma katika mikakati mbalimbal.i ya uzalishaji, mali, kuondoa njaa na Umasikini.
· Atakuwa ni Katibu wa kamati ya maendeleo ya kata.
· Ataratibu na kusimamia upangaji wa shughuli za maendeleo ya kata, vijiji na Mtaa.
· Atatafsiri sera na kusimamia utekelezaji wa sheria ndogondogo katika Kata yake.Atamsaidia Mkurugenzi Kuratibu na kusimamia shughuli za Uchaguzi katika Kata.
· Kumsaidia na kumwakilisha Mkurugenzi katika kusimamia maendeleo ya eneo lake.
· Kusimamia utendaji kazi wa wataalamu na watendaji wengine katikangazi ya Kata.
· Kuratibu na kuandaa taarifa za utekelezaji na kuziwasilisha kwa mkurugenzi na nakala kwa Katibu Tarafa.
· Atakuwa mwenyekiti katika vikao vinavyowahusisha wataalamu na watendaji wa vjiji, na NGO’S katika kata yake.
· Atakuwa Msimamizi na mratibu wa takwimu zote zinazokusanywa katika vijiji, vitongoji, na kata yake.
38
63.2 SIFA ZA MWOMBAJI.
· Kuajiriwa wenye Shahada ya Sanaa yenye mwelekeo wa Sayansi ya Jamii (Social Sciences) Utawala, (Public Administration and Local Gorvernment), Sheria au Sifa nyingine inayolingana na hizo kutoka Chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali.
63.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGS D. kwa mwezi.
64.0 AFISA MTENDAJI WA KATA DARAJA LA III (WARD EXECUTIVE OFFICER GRADE III) – NAFASI 91
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Halmashauri ya Manispaa ya Singida, Kigoma/Ujiji na Songea, Halmshauri ya Wilaya ya Chato, Songea, Handeni, Kibondo, Mkinga, Tunduru, Mbeya, Mkuranga, Kibaha, Kwimba, Njombe, Rufiji, Bukoba, Mwanga, Sengerema na Mpanda
64.1 MAJUKUMU YA KAZI
· Atakuwa Mtendaji Mkuu wa Kata na kiungo cha Uongozi kwa Idara zote katika kata na atashughulikia masuala yote ya kata
· Atakuwa Mhamasishaji mkuu wa Umma katika mikakati mbalimbali ya uzalishaji, mali, kuondoa njaa na Umasikini.
· Atakuwa ni Katibu wa kamati ya maendeleo ya kata.
· Ataratibu na kusimamia upangaji wa shughuli za maendeleo ya kata, vijiji na vitongoji.
· Atatafsiri sera na kusimamia utekelezaji wa sheria ndogondogo katika Kata yake.Atamsaidia Mkurugenzi Kuratibuna kusimamia shughuli za Uchaguzi katika Kata.
· Kumsaidia na kumwakilisha Mkurugenzi katika kusimamia maendeleo ya eneo lake.
· Kusimamia utendaji kazi wa wataalamu na watendaji wengine katika ngazi ya Kata.
· Kuratibu na kuandaa taarifa za utekelezaji na kuziwasilisha kwa mkurugenzi na nakala kwa Katibu Tarafa.
· Atakuwa mwenyekiti katika vikao vya vinavyowahusisha wataalamu na watendaji wa vjiji, na NGO’S katika kata yake.
· Atakuwa Msimamizi na mratibu wa takwimu zote zinazokusanywa katika vijiji, vitongoji, na kata yake.
64.2 SIFA ZA MWOMBAJI.
· Kuajiriwa waliohitimu kidato cha nne au sita na kuhudhuria mafunzo ya Stashahada yenye mwelekeo wa Sayansi ya Jamii (Social Sciences) Utawala, (Public Administration and Local Gorvernment), Stashahada ya Sheria au Sifa nyingine inayolingana na hizo kutoka Chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali.
64.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia viwango vya Serikali ngazi ya Mshahara TGS C kwa mwezi. 39
65.0 AFISA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA II (VILLAGE EXECUTIVE OFFICER GRADE II) – NAFASI 57
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Waajiri wafuatao:- Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, Kondoa, Tandahimba,Wilaya ya Mbeya, Babati, Mkuranga, Simanjiro, Newala na Ruangwa
65.1 MAJUKUMU YA KAZI
· Atakuwa Mtendaji na Mshauri Mkuu wa Serikali ya Kijiji na Kamati zake katika Mipango ya Maendeleo ya kijamii na Utekelezaji wa Mipango ya Maendeleo.
· Atakuwa Afisa Mhasibu wa Serikali ya Kijiji na atasimamia mapato na matumizi ya Serikali ya kijiji
· Atakuwa Mlinzi wa Amani na Msimamizi wa Utawala Bora katika Kijiji.
· Ataratibu na kusimamia upangaji wa utekelezaji wa Mipango ya Maendeleo ya kijiji
· Atakuwa Katibu wa Kamati ya Halmashauri ya Kijiji.
· Atatafsiri Sera, ataratibu na kusimamia utekelezaji wa Sheria ndogondogo za Halmashauri ya Kijiji.
· Ataratibu na kuandaa taarifa ya utekelezaji wa kazi katika eneo lake na kuziwasilisha kwenye Halimashauri ya Kijiji na baadae kwenye kata .
· Ataongoza vikao vya maendeleo ya Kijiji vitavyowahusisha wananchi na wataalamu waliopo kwenye eneo lake.
· Atahamasisha wananchi katika kampeni za kuondoa njaa, umasikini, na kuongeza uzalishaji mali.
· Atasimamia matumizi bora ya Nguvu kazi.
· Atakuwa Kiongozi wa Wakuu wa Vitengo vya Kitaalamu Katika Kijiji.
· Atasimamia ukusanyaji wa kumbukumbu za walipa kodi, wataalamu mbalimbali na NGO waliopo katika kijiji.
65.2 SIFA ZA MWOMBAJI.
· Kuajiriwa wenye elimu ya kidato cha IV na VI waliohitimu Stashahada ya kawaida katika fani yoyote yenye mwelekeo wa Sayansi ya Jamii (Social Sciences) Utawala, (Public Administration and Local Gorvernment), Stashahada ya Sheria au Sifa nyingine inayolingana na hizo kutoka Chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali.
65.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia viwango vya Serikali ngazi ya Mshahara TGS C kwa mwezi.
66.0 AFISA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III (VILLAGE EXECUTIVE OFFICER GRADE III) – NAFASI 207
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Waajiri wafuatao:- Halmashauri ya Manispaa ya Singida, Halmashauri ya Mji Njombe, Halmashauri ya Wilaya ya Chato, Handeni, Mkinga, Sengerema, Tunduru, Babati, Masasi, Mtwara, Mwanga, Kwimba, Rufiji, Ngara, Tarime na Mpanda 40
66.1 MAJUKUMU YA KAZI
· Atakuwa Mtendaji na Mshauri Mkuu wa Serikali ya Kijiji na Kamati zake katika Mipango ya Maendeleo ya kijamii na Utekelezaji wa Mipango ya Maendeleo.
· Atakuwa Afisa Mhasibu wa Serikali ya Kijiji na atasimamia mapato na matumizi ya Serikali ya kijiji
· Atakuwa Mlinzi wa Amani na Msimamizi wa Utawala Bora katika Kijiji.
· Ataratibu na kusimamia upangaji wa utekelezaji wa Mipango ya Maendeleo ya kijiji
· Atakuwa Katibu wa Kamati ya Halmashauri ya Kijiji.
· Atatafsiri Sera, ataratibu na kusimamia utekelezaji wa Sheria ndogondogo za Halmashauri ya Kijiji.
· Ataratibu na kuandaa taarifa ya utekelezaji wa kazi katika eneo lake na kuziwasilisha kwenye Halimashauri ya Kijiji na baadae kwenye kata.
· Ataongoza vikao vya maendeleo ya Kijiji vitavyowahusisha wananchi na wataalamu waliopo kwenye eneo lake.
· Atahamasisha wananchi katika kampeni za kuondoa njaa, umasikini, na kuongeza uzalishaji mali.
· Atasimamia matumizi bora ya Nguvu kazi.
· Atakuwa Kiongozi wa Wakuu wa Vitengo vya Kitaalamu Katika Kijiji.
· Atasimamia ukusanyaji wa kumbukumbu za walipa kodi, wataalamu mbalimbali na NGO waliopo katika kijiji.
66.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wenye Elimu ya Kidato cha Nne au cha sita waliohitimu Astashahada (Certificate) katika Fani yoyote yenye mwelekeo wa Sayansi ya Jamii (Social Sciences) Utawala, (Public Administration and Local Gorvernment), Astashahada ya Sheria au Sifa nyingine inayolingana na hizo kutoka Chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali.
66.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGS B kwa mwezi.
67.0 AFISA MTENDAJI MTAA II (MTAA EXECUTIVE OFFICER GRADE II) – NAFASI 36
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Halmashauri ya Manispaa ya Temeke, Halmashauri ya Manispaa ya Songea na Sumbawanga
67.1 MAJUKUMU YA KAZI
· Kutoa ushauri katika utekelezaji wa sheria za Serikali za Mitaa.
· Kutoa ushauri juu ya uanzishaji na uendeshaji wa mamlaka mpya za Serikali za Mitaa.
· Kutoa ushauri juu ya makadirio ya mapato na matumizi ya Serikali za Mitaa.
· Kusimamia na kushauri juu ya matumizi bora ya fedha za Serikali.
· Kutayarisha taarifa za robo mwaka na mwaka zinazohusu mwenendo wa Serikali za Mitaa.
41
· Kufanya kazi nyingine zitakazoagizwa na Watendaji, Wasimamizi wa masuala ya Serikali za Mitaa.
67.2 SIFA ZA MWOMBAJI
· Kuajiriwa waliohitimu kidato cha nne au sita na kuhudhuria mafunzo ya Stashahada ya yenye mwelekeo wa Sayansi ya Jamii (Social Sciences) Utawala, (Public Administration and Local Gorvernment), Stashahada ya Sheria au Sifa nyingine inayolingana na hizo kutoka Chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali.
67.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia viwango vya Serikali ngazi ya Mshahara TGS.C kwa mwezi.
68.0 AFISA MTENDAJI MTAA DARAJA LA III (MTAA EXECUTIVE OFFICER GRADE III) – NAFASI 46
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma, Morogoro, Mtwara, Kigoma/Ujiji na Singida na Halmashauri ya Wilaya ya Rufiji.
68.1 MAJUKUMU YA KAZI
· Atakuwa Mtendaji na Mshauri Mkuu wa Serikali ya Mtaa na Kamati zake katika Mipango ya Maendeleo ya kijamii na Utekelezaji wa Mipango ya Maendeleo.
· Atakuwa Afisa Mhasibu wa Serikali ya Mtaa na atasimamia mapato na matumizi ya Serikali ya Mtaa
· Atakuwa Mlinzi wa Amani na Msimamizi wa Utawala Bora katika Mtaa
· Ataratibu na kusimamia upangaji wa utekelezaji wa Mipango ya Maendeleo ya Mtaa
· Atakuwa Katibu wa Kamati ya Halmashauri ya Mtaa.
· Atatafsiri Sera, ataratibu na kusimamia utekelezaji wa Sheria ndogondogo za Halmashauri ya Mtaa
· Ataratibu na kuandaa taarifa ya utekelezaji wa kazi katika eneo lake na kuziwasilisha kwenye Halimashauri ya Mtaa na baadae kwenye Kata.
· Ataongoza vikao vya maendeleo ya Mtaa vitavyowahusisha wananchi na wataalamu waliopo kwenye eneo lake.
· Atahamasisha wananchi katika kampeni za kuondoa njaa, umasikini, na kuongeza uzalishaji mali.
· Atasimamia matumizi bora ya Nguvu kazi.
· Atakuwa Kiongozi wa Wakuu wa Vitengo vya Kitaalamu Katika Mtaa.
· Atasimamia ukusanyaji wa kumbukumbu za walipa kodi, wataalamu mbalimbali na NGO waliopo katika Mtaa.
68.2 SIFA ZA MWOMBAJI
· Kuajiriwa wenye Elimu ya Kidato cha Nne au cha sita waliohitimu Astashahada (Diploma) katika Fani yoyote yenye mwelekeo wa Sayansi ya Jamii (Social Sciences) Utawala, (Public Administration and Local Gorvernment), Atashahada ya Sheria au
42
Sifa nyingine inayolingana na hizo kutoka Chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali.
68.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia viwango vya Serikali ngazi ya Mshahara TGS B kwa mwezi.
69.0 AFISA USTAWI WA JAMII DARAJA LA II (SOCIAL WELFARE OFFICER GRADE II) – NAFASI 25
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Waajiri wafuatao: – Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Katibu Tawala Mkoa wa Pwani, Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, Singida, Sumbawanga, Halmashauri ya Wilaya ya Babati, Handeni, Mkinga, Newala, Tandahimba, Bahi na Chamwino na Halmashauri ya Jiji la Mwanza
69.1 MAJUKUMU YA KAZI
· Kuendesha Usaili wa wahudumia (watu wenye ulemavu, wazee, familia zenye matatizo, watoto na vijana wenye matatizo mbalimbali).
· Kufanya ukaguzi wa mazingira wanayoishi wahudumiwa ili kupata taarifa zao kamili
· Kuandaa taarifa za usaili na ukaguzi wa mazingira ya wahudumiwa.
· Kupokea na kukusanya taarifa za Ustawi wa Jamii kutoka kwa wadau na vituo mbalimbali vya Ustawi wa Jamii.
· Kupokea na kukusanya takwimu zinazohusu huduma za watu wenye ulemavu, wazee, malezi ya watoto na familia zenye matatizo.
· Kupokea, kuchambua na kuandaa orodha ya maombi ya uandikishaji vituo vya kulelea watoto wadogo mchana, malezi ya kambo (foster care) na vituo vya walezi wa watoto wadogo mchana.
· Kupokea, kuchambua na kuandaa orodha ya maombi ya msaada wa Rais kutoka kwa akina mama, walojifungua watoto watatu au zaidi kwa mara moja.
· Kupokea, kuchambua na kuandaa orodha ya maombi ya watoto yatima au wanaohitaji misaada mbalimbali
· Kupokea, kuchambua na kuandaa orodha ya maombi mbalimbali toka kwenye familia za watu wenye dhiki
· Kuhoji na kuandaa taarifa za washitakiwa.
· Kusimamia wahudumiwa katika makazi, vyuo vya mafunzo ya Ufundi Stadi vya watu wenye ulemavu, Mahabusu za watoto na shule za maadilisho.
· Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi zinazohusiana na elimu, uzoefu na ujuzi wake.
69.2 SIFA ZA MWOMBAJI
· Kuajiriwa wenye Shahada ya BA (Social Works or Sociology) au Stashahada ya juu ya Ustawi wa Jamii (Advanced Diploma in Social Works) kutoka Chuo cha elimu ya juu kinachotambuliwa na Serikali
43
69.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS D kwa mwezi.
70.0 MSAIDIZI USTAWI WA JAMII DARAJA LA II (SOCIAL WELFARE ASSISTANT GRADE II) – NAFASI 6
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga, Ruangwa
70.1 MAJUKUMU YA KAZI
· Kutambua na kuhudumia watu walio katika makundi maalum na mazingira hatarishi.
· Kukusnya takwimu zinazohusu watu walio katika makundi maalum na mazingira hatarishi.
· Kuchambua na kuandaa orodha ya maombi mbalimbali kutoka kwenye familia na watu wenye dhiki.
· Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi zinazohusiana na elimu, uzoefu na ujuzi wake.
70.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha nne au sita wenye cheti cha mafunzo ya mwaka mmoja ya Ustawi wa Jamii kutoka Chuo kinachotambuliwa na Serikali
70.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali TGS C kwa mwezi.
NB: MASHARITI YA JUMLA KWA KAZI ZOTE.
i. Waombaji wote wawe ni Raia wa Tanzania.
ii. Waombaji wote waambatishe cheti cha kuzaliwa.
iii. Waombaji ambao tayari ni watumishi wa Umma na wamejipatia sifa za kuingilia katika kada tofauti na walizonazo, wapitishe barua zao za maombi ya nafasi za kazi kwa waajiri wao na Waajiri wajiridhishe ipasavyo.
iv. Nafasi ya kazi inayoombwa iandikwe katika kichwa cha habari cha barua na juu ya bahasha, kutozingatiwa hili kutasababisha maombi ya kazi kuwa batili.
v. Waombaji waambatishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detailed C.V) yenye anwani na namba za simu za kuaminika pamoja na majina ya wadhamini (referees) watatu wa kuaminika.

vi. Maombi yote yaambatane na vyeti vya taaluma, maelezo, nakala za vyeti vya kidato cha nne na kidato cha sita kwawale waliofikia kiwango hicho na vyeti vya kuhitimu mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika. Viambatanisho hivyo vibanwe sawa sawa kuondoa uwezekano wa kudondoka kupotea.
- Postgraduate/Degree/Advanced Diploma/Diploma/Certificates.
- Cheti cha mtihani wa kidato cha IV na VI
- Computer Certificate
- Vyeti vya kitaaluma (Professional certificates from respective boards)
- Picha moja “Passport size” ya hivi karibuni iandikwe jina kwa nyuma.
vii. “Transcripts”, “Testmonials”, “Provisional Results”, “Statement of results”, hati matokeo za kidato cha nne na sita (FORM IV AND FORM VI RESULTS SLIPS) HAVITAKUBALIWA.
viii. Waombaji wawe na umri usiozidi miaka 45.
ix. Waombaji waliostaafishwa katika Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kama wanakibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.
x. Waombaji kazi ambao tayari ni waajiriwa katika nafasi za kuingilia walioko katika utumishi wa umma wasiombe na wanatakiwa kuzingatia maelekezo yaliyo katika Waraka Na CAC. 45/257/01/D/140 wa tarehe 30 Novemba 2010.
xi. Uwasilishaji wa taarifa na sifa za kugushi wahusika watachukuliwa hatua za kisheria.
xii. WAAJIRI WOTE WALIOPO NJE YA DAR ES SALAAM WANAOMBWA KUSAMBAZA MATANGAZO HAYA KWENYE MBAO ZA MATANGAZO NA MAENEO MENGINE.
xiii. Mwisho wa kupokea barua za maombi ni tarehe 8 Juni, 2013
xiv. Aidha, uwasilishaji wa barua kwa mkono katika ofisi za Sekretarieti ya ajira HAURUHUSIWI.
xv. Maombi yanaweza kuandikwa kwa Lugha ya Kiswahili au Kiingereza na yatumwe kupitia posta kwa anuani ifuatayo.
Secretary,
Public Service Recruitment
Secretariat,
P.O.Box 63100
Dar es Salaam.

AU

Katibu,
Sekretariati ya Ajira katika
Utumishi wa Umma,
SLP.63100,