Showing posts with label ajira. Show all posts
Showing posts with label ajira. Show all posts

November 16, 2017

MV NJOMBE INAVYOFUNGUA FURSA KWA WAKAZI ZIWA NYASA.


Honorius Mpangala, 0628994409

NA. HONORIUS MPANGALA
AKIWA katika kampeni za urais mwaka 2005 Rais mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete katika ardhi ya Kyela Mkoani Mbeya alihaidi meli. Alirudia tena kauli hiyo alipokuwa katika ardhi ya Mbamba Bay Mkoani Ruvuma. Baada ya kipindi cha utawala wake hatimaye meli alizoahidi tayari zimeonwa na Wanyasa. 

MV Njombe imekamilika na kufanikiwa safari moja ya majaribio kutoka Bandari ya Itungi hadi Mbamba Bay.  Yapo mambo ambayo ni fursa kwa wakazi wa Nyasa kutokana Meli hii. Kama inavyoitwa ni meli ya mizigo ni chombo kitakachoweza kuwainua kiuchumi wakaza wa Nyasa kama watakitumika ipasavyo. Kuinuka kiuchumi kutatokana na kujikita katika shughuli ambazo wakazi wake watajishughulisha na shughuli kama ilivyo kilimo biashara na hata ufugaji wa kisasa na wenye tija katika maisha ya leo.
Kilimo cha biashara ni moja ya ujasiriamali ambao watu wengi wamekuwa wakijishughulisha nao. Katika mwambao wa Ziwa Nyasa hususani wilaya Nyasa yapo mabonde ambayo yanaweza kufanyika kilimo cha mazao ya muda mfupi na kwa mfumo wa kilimo cha umwagiliaji, na kile cha kutegema mvua na kuleta tija.


November 13, 2017

KWANINI SEKRETARIETI YA AJIRA HAINA MATAWI NCHINI?

NA MARKUS MPANGALA
MIAKA kadhaa iliyopita nilishindwa kuwaelewa kabisa watendaji wa Wakala  wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) hapa nchini. Nilikuwa siwaelewi kwa sababu siku moja niliwahushudia wafanyabiashara fulani kutoka Songea mkoani Ruvuma, wakizunguka vyumba vya ofisi vya taasisi hiyo kwenye jengo la Ushirika liliko Barabara ya Lumumba, Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam kwa madhumuni ya kusajili kampuni yao.  
Jenista Mhagama

Pili,niliwahi kumsaidia rafiki yangu, Albert Nyaluke Sanga, ambaye ni mfanyabiashara mkubwa mkoani Iringa, ili apate leseni ya biashara. Haikuwa leseni yake binafsi, bali aliamua kumsaidia kijana mmoja aliyekuwa na ndoto za kuwa mfanyabiashara, lakini alikosa pa kunzia.
Rafiki yangu huyo anapenda kuwasaidia vijana wanaojishughulisha na ujasiriamali kwa sababu anaamini hiyo ndiyo njia pekee ya kuwakomboa, badala ya elimu yao na kuondokana na matembezi ya kusambaza bahasha za kuomba nafasi za kazi.

November 03, 2017

UCHAMBUZI WA KITABU: IT CAN'T BE TRUE



KITABU: IT CAN’T BE TRUE
MWANDISHI: JOHN MWAKYUSA
MCHAMBUZI: MARKUS MPANGALA

HII ni mara yangu ya kwanza kusoma riwaya ya mwandishi John R.P. Mwakyusa, mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam. Riwaya inaitwa “It Can’t Be True: A Story from Uganda-the Pearl of Africa”, na kuchapishwa kwa mara ya kwanza mwaka 2017 na kampuni ya Partridge Publishing ya India.

October 17, 2017

MAONI YA MHARIRI: KWA WILAYA YA NYASA DUNIA HAIJABADILIKA?

Majuzi nimeona picha ya mwanadada mashuhuri katika mtandao wa Instagram, Mange Kimambi akionyesha majengo ya hospitali ya Lumeme wilayani Nyasa ikiwa na mazingira mabaya ya kufanyia kazi na ukosefu wa huduma muhumu. Pamoja na jengo lenyewe kutokamilika, lakini limekuwa likitumika hivyo hivyo.

Kwangu mimi ile ilikuwa habari kubwa sana kwa wilaya yetu ya Nyasa. Kama mwanahabari naamini kuripotiwa matukio au masuala yasiyofaa  ndani ya jamii ambayo haitoi habari za kutosha ni njia mojawapo kubwa ya kubadili mwenendo.

HAPA CHINI kuna Blogu ya JIMBO LA NYASA. Lakini habari za Jimbo husika ziliwekwa mara ya mwisho Januari mwaka huu. Nimejiuliza wasaidizi wa Mbunge wanafanya nini kama hawawezi kutoa taarifa za ofisi ya mbunge? Najiuliza hivi hatuoni umuhimu wa habari zetu zikiwa hadharani bila kujali mbaya au nzuri?

Je waanzilishi wa blogu ya JIMBO walikusudia tamasha au nini? BONYEZA HAPA KUTAZAMA.  Kimsingi habari za Jimbo la Nyasa ni lazima zitolewe wala kwa wananchi. Pili inadhihirisha "kuamini" kuwa NYASA ni ileile ambayo inaishi pasipo kuwa na habari zozote. Mtazamo huo si sahihi ndio maana wahusika wanaona "bora liende tu" huku wakisahau na kushindwa "KUMUUZA" mbunge. 

Nimejiuliza hadi leo hata kutengeneza ukurasa wa habari za mbunge kwenye mitandao hatuwezi kweli?  Hivi mahusiano ya mbunge na wapigakura wake yana maana gani? Naandika hapa kwasababu naamini wapo wahusika wanaofikisha ujumbe. Ningependa kuwakumbusheni kuwa "kutomuuza mbunge" katika ulimwengu wa kidigitali ni uzembe. Labda tunaweza kutembelea wananchi kila kona ya jimbo, lakini tunapawa kuelewa kuwa taarifa za huko ziwekwe sehemu maalumu kutunza kumbukumbu sio mambo ya "MASJALA" tena (hizo ni zama za kale mawe).

Kwa heshima nawakumbusha wasaidizi wa mbunge, kutoitendea haki blogu, kutozungumzia hata utalii ambao ni chachu ya kukuza mzunguko wa fedha wilayani kwetu ni UDHAIFU unaopaswa kurekebishwa.
Ninawatakieni majukumu mema. 
HABARI NI BIASHARA. HABARI NI UCHUMI.

MARKUS MPANGALA,
Oktoba 17/ 2017
Dar es salaam

September 10, 2013

WATANZANIA TUKAZANE KUWEKEZA KWENYE ARDHI



Na, Albert Sanga, Iringa
 
Leo ni mwaka mmoja kamili umepita tangu nilipoandika makala hapa safuni iliyokuwa na kichwa, “Njooni shambani mtajirike”. Ilikuwa ni makala iliyotoa shime kwa watanzania kuchangamkia fursa ya uwekezaji kwenye kilimo cha miti.

Katika makala ile niliwaeleza watanzania upana wa faida ya kuwekeza katika miti aina mbalimbali huku nikijikita katika miti ya mbao, karatasi na nguzo.  Nilichambua kwa kina sana gharama za upandaji wa miti hiyo, muda wa kuvuna, soko lake lilivyo na matarajio ya biashara hiyo kwa miaka ya baadae.

Leo ninaandika tena makala hii huku nikiwa na furaha tele moyoni mwangu kwa sababu makumi ya watanzania waliuitikia mwito wangu na wakachangamkia fursa hii. Kama ambavyo nilitamani iwe, ndivyo ilivyokuwa kwani wengi wamenijulisha kuwa hawakulazia damu, walichangamka na kuanza kuwekeza.
Ingawa mimi ni mmoja ya watanzania ambao wanajishughulisha na uwekezaji katika mashamba ya miti mkoani Iringa, kiu yangu ilikuwa ni kuona watu wakichangamkia fursa hii mahali kokote inakopatikana. Mikoa ya Tanga, Njombe, Mtwara, Tabora, Mbeya, Bukoba na kwingine kwingi kunastawi miti ya aina mbalimbali.

Kwa hakika wengi wameendelea kufanya hivyo kwani wamekuwa wakinijulisha. Wapo makumi waliosafiri hadi hapa Iringa kujifunza na kujionea fursa hii inavyowanufaisha na kuwatajirisha watu; kati yao wapo walioamua kuanza kuwekeza na wapo ambao walirudi makwao ili kujipanga kwa ajili ya kuwekeza wakati ujao. 

Furaha yangu ilikuwa kubwa zaidi pale ambapo wapo waliofika kujifunza hapa Iringa kasha wakaenda katika maeneo yao na kuanza kuwekeza. Wapo mamia ambao walizungumza nami kwa simu kutoka maeneo mbalimbali wakiwa wamevutiwa na habari zile.  

Nami kwa moyo mkunjufu nilishirikishana nao uzoefu wangu na kuwahamasisha waanze hata kama ni kidogo kidogo mahali popote wanapoona inafaa. Ni jambo la kujivunia na la fahari kutamka kwamba makala ile imekuwa na ‘impact’ kubwa mno kwa mamia ya watanzania ambao walihamasika kuanza kuwekeza katika miti kule Tanga, Tabora, Mbeya, Mtwara, Morogoro na wengine wengi hapa Iringa.

Kama ambavyo nimekuwa nikisema mara kwa mara katika makala zangu; ni kwamba muda wa kulalamika lalamika umekwisha. Mazoea na utamaduni wa watanzania wengi kudhani kwamba tunaonewa wakati wote haujatusaidia mpaka hapa kwa jinsi hii hakuna sababu ya kuendelea nao. 

Mtindo wa kuishi maisha ya kutaka kuhurumiwa yanatupotezea muda wenye thamani. Tumekuwa tukilalamika kuwa wageni (wanaokuja kwa jina la wawekezaji) wanatupora ardhi; lakini tusichokitafakari ni hiki, “Mimi kama mtanzania kwa nafsi yangu na kwa uwezo wangu nimefanya nini cha maana katika ardhi ninayoweza kuipata hapa nchini ama ninayomiliki?”.

Bahati nzuri ni kwamba idadi kubwa ya watanzania tunafahamu kuwa ardhi ni utajiri; lakini hatufanyi juhudi za makusudi kuuvumbua na kuutumia utajiri huo. Tunayo mamilioni ya hekta za ardhi zenye rutuba na zinazofaa kwa kilimo cha aina mbalimbali lakini bidii zetu hazijatosha hata tufike mahali tuseme ardhi haitutoshi.

Itakumbukwa kuwa wakati nikiandika makala ile mwaka jana pia nilizindua kampeni ya kimazingira niliyoibatiza jina la “Green The World And Become Rich”.  Kimsingi kampeni hii nililenga kuwahamasisha watanzania washiriki kikamilifu katika utunzaji wa mazingira na wakati huo huo wakitengeneza utajiri. 

Unapochukua fedha yako na kuwekeza kwenye shamba la miti moja kwa moja unakuwa umetunza mazingira kupitia miti uliyopanda lakini pia usiku na mchana kadiri miti inavyoendelea kukua unakuwa ukitengeneza mamilioni. 

Na hii ni namna moja nzuri ambayo watanzania tunaweza kuwekeza kwenye ardhi. Leo unapanda miti inakaa miaka saba ama kumi unavuna halafu baada ya hapo ardhi yako unaitafutia matumizi mengine. Si hivyo tu, lakini katika hiki hiki kilimo cha miti; ndani ya shamba lako unaweza kufuga nyuki, ukawa unavuna asali hukuku ukisubiri kuvuna miti yako.
Msukumo wa kuanzisha kampeni hii ya “Green The World And Become Rich” niliupata baada ya kutafakari nafasi walizonazo watu wengi wenye nia ya kuwekeza katika kilimo cha miti na katika ardhi kwa ujumla. Nilifahamu kuwa sio rahisi sana kwa mtu kutumia fedha zake na kupanda miti kwa faida moja tu ya kutunza mazingira. 

Nilijaribu kufikiri namna ya kuongeza thamani; hivyo ilinibidi nifanye kazi ya kuwaelimisha watu mbalimbali mambo mengi kuhusu miti, biashara yake na namna inavyolipa. Ninafahamu kuwa mamia ya wanaoendelea kuwekeza kwenye miti sehemu mbalimbali Tanzania, kufuatia kampeni yangu; wanawezekeza kwa mtazamo wa kupata faida kifedha huko mbeleni. 

Hilo ni jema sana lakini wakati huo huo mimi na wadau wengine wa mazingira tunashangilia kwa sababu mazingira yanaimarika huku watu wakitajirika. Vile vile Nilitambua kuwa wengi wanaweza wasiwe na taarifa sahihi kuhusu kilimo hiki, kwa maana ya maeneo kinakostawi, taratibu za upataji maeneo, lakini kubwa kuliko yote ni namna ya usimamiaji pindi wakiwa mbali. 

Nilifahamu mtu angeweza kujiuliza maswali mengi yakiwemo; “Nitawezaje kumiliki shamba Tabora wakati mimi kikazi nipo DaresSalaam?”, “Nitawezaje kufahamu biashara ya mbao, magogo, pindi ukifika muda wa kuvuna?”, “ Mbali na faida nitajuaje gharama za uendeshaji na je nitazimudu?”.  

Katika kampeni hii kulikuwa na majibu yote ambao kwa wale waliovutiwa kuwekeza Iringa katika maeneo inakowekeza kampuni yangu, nilijitolea kuwapa usaidizi wa kuwatunzia na kuyahudumia mashamba yao. Fursa bado zipo nyingi, watanzania wenzangu tusilale.
Ninapoandika makala haya leo ninatumia wasaa huu kuwakumbusha wale jamaa zangu wa kule Tanga, Tabora, Mbeya na kwingine ambao waliniahidi kuwa wataanza kuwekeza katika maeneo yao mwakani (yaani mwaka huu). 

Msimu ndio umeanza, kuandaa mashamba, kuaandaa miche na maandalizi mengine. Hapo hapo mlipo fanyeni kitu katika ardhi zenu, wekezeni kwa manufaa yenu na ya watoto wenu, isaidieni dunia kwa kuboresha mazingira yake.

Wale waliofika Iringa wengi wao nilikuwa ninawapa zawadi ya nakala ya sheria ya ardhi ya mwaka 1999. Na wengine waliokuwa wakiwasiliana nami nilikuwa ninawapa semina fupi kuhusu sheria ya ardhi. Kiujumla sheria hii inatupendelea mno wazawa tofauti na malalamiko mengi ambayo huwa ninayasikia.

Pengine Watanzania tuna tatizo katika ubunifu na inapotokea wengine wamebuni tunakuwa wepesi wa kudhani wametuibia. Mathalani, tunaishi na ardhi tusiyoifanyia kazi miaka nenda rudi, akitokea mwekezaji akabuni mradi Fulani katika ardhi hiyo; tunaanza kuja juu! Hatujiulizi tulikuwa wapi na kwa nini hatukuchangamkia?

Kingine kinachotumaliza Watanzania wengi ni ile dhana ya kudhani kuwa kilimo ni utumwa, shamba tunaona ni kwa ajili ya waganga njaa na waliokosa nafasi ya kupata ajira nzuri. Hii ni dhana mbaya na inachangia sana watanzania kutokuwa na mikakati ya kuitumia ardhi kikamilifu. 

Hata hivyo nikiri kuwa wapo watanzania ambao wanatambua thamani ya ardhi na wanaitumia ardhi vizuri kwa uzalishaji na uwekezaji wenye tija. Lakini idadi hiyo haitoshi ukilinganisha na idadi ya wasiotambua nguvu na utajiri wa ardhi ambao wanaendelea kulalamika ugumu wa maisha na waliopoteza tumaini.

Jambo jingine linalotumaliza watanzania ni kutokuwa na maono ya muda mrefu. Wengi wetu tunataka mambo ya papo kwa papo, hatupendi kuangalia mambo ya vipindi virefu mbele. Mfano mzuri ni katika hili la uwekezaji katika ardhi. 

Mtu anaona ni kupoteza fedha kununua shamba leo ambalo pengine linaweza kuja kutumika miaka ishirini huko baadae. Mtu anaona ni kama kupoteza fedha kupanda miti leo ambayo atakuja kuivuna miaka saba ama miaka kumi ijayo. 

Wasichokumbuka wengi ni kuwa unachopuuza kufanya leo kwa gharama ndogo miaka ishirini ama kumi ijayo hutakuwa na uwezo wa kukifanya hata kama ukitamani. Mzee wangu mmoja hapa Iringa alinisimulia namna alivyopuuza kununua kiwanja kimoja hapa mjini Iringa mtaa wa Miyomboni mwaka 1994. 

Wakati huo anasema kiwanja hicho kilikuwa kikiuzwa kwa shilingi laki nne; lakini mwaka jana, 2012 kimeuzwa kwa milioni 320! Mzee wangu huyu anasema mwaka huo 1994 laki nne kwake zilikuwa ni hela ndogo sana lakini akapuuza. Leo hii miaka 20 baadae kiwanja kile kile kimeuzwa mara mia nane ya bei aliyoipuuza ilhali yeye (mzee wangu huyu) leo hana hata ujanja wa kupata milioni kumi! 

Kwa maneno yake anasema, “Ningekuwa na mipango ya muda mrefu katika kuwekeza kwenye viwanja, ardhi na mashamba, leo mimi ningekuwa milionea hapa mjini” Anachofanya mzee wangu huyu ni utekelezaji wa ule msemo, “Majuto ni mjukuu”!
Watanzania tusilale, ushindi wetu kiuchumi umo ardhini!
stepwiseexpert@gmail.com +255 719 127 901

December 19, 2012

HALI YA WAVUVI NA UVUVI KATIKA ZIWA NYASA WILAYANI NYASA

Mvuvi akiwa na zana zake za kazi. 
PICHA: kwa hisani ya kaka Francis Godwin

UHABA wa samaki ziwa Nyasa upande wa Tanzania unaochangiwa na vifaa duni vya uvuvi umepelekea baadhi ya wanaume wa tarafa ya Mwambao wilaya ya Ludewa mkoani Iringa kutelekeza familia na kwenda nchini Malawi kufanya shughuli za uvuvi kama njia ya kukwepa changamoto za uchumi zinazoendelea kuwa kikwazo katika wilaya hiyo.
Uchumi wa wananchi wa tarafa yaMwambao ambao ulikuwa ukitokana na ajira ya uvuvi kwenye ziwa Nyasa nao umezidi kuporomoka kwa kasi kubwa na kupelekea hata biashara za wananchi wa maeneo hayo ambazo zilianzishwa kutokana na wingi wa wageni waliokuwa wakifika kujumua samaki kwenye ziwa hilo pia kuathirika kwa kiasi kikubwa.
Kama inavyofahamika kuwa uvuvi wa samaki kwa wananchi wa tarafa ya Mwambao wilayani Ludewa ndio shughuli kubwa ya kiuchumi ambayo imekuwa ikitegemewa na karibu robo tatu ya wakazi wa tarafa hii ya Mwambao na ndio shughuli iliyopelekea tarafa hiyo kuwa na mzunguko mkubwa wa fedha hasa kipindi cha nyuma japo kwa sasa imeanza kubaki historia pekee. 
Bonyeza kiungo;    SOMA ZAIDI HAPA

December 02, 2012

TAARIFA KWA WAWEKEZAJI WAPYA KATIKA KILIMO CHA MITI YA MBAO, KARATASI NA NGUZO.

Fresh Farms & Tours (T), biashara tanzu ya Anesa Co.,Ltd (Nyaluke Business Empire); inayojishughulisha na upandaji, utunzaji na uendelezaji wa mashamba ya miti ya mbao, karatasi na nguzo-mkoani Iringa. Pia inahusika na uvunaji na usambazaji wa mazao ya miti, (mbao na nguzo za umeme) sambamba na ufugaji.
Fresh Farms ilianzisha programu maalumu, mapema mwaka jana; inayolenga kuwawezesha watanzania wengine kuwekeza katika kilimo cha miti kwa urahisi. Tayari makumi wa watanzania wamechangamkia fursa hii. Fresh Farms & Tours (T) tunapenda kuwaarifu wale wote wenye nia ya kuwekeza nasi; KWAMBA kuanzia tar 1, Feb, 2013 kutakuwa na mabadiliko ya bei na gharama za uendeshaji kwa mashamba ya miti. Mashamba tunayoyauza laki sita kwa sasa; bei mpya itakuwa milioni moja; na yale tunayouza laki nane gharama yake itakuwa milioni moja na nusu.
Bei hizi hazitawaathiri wateja wa awali na wale ambao wamekwisha wasilisha oda zao. Fresh Farms & Tours (T) tunaendelea kuboresha huduma, taarifa na usaidizi kwa wote wanaowekeza nasi. Kabla ya mwisho wa mwaka huu; tutazindua tovuti maalaumu itakayobeba taarifa za uwekezaji katika kilimo na ufugaji; pia kila anaewekeza nasi atapata nafasi ya kufungua akaunti yake katika tovuti hiyo; na akaunti hiyo itamwezesha kufuatilia mwenendo wa mashamba yake popote alipo duniani. Fresh Farms & Tours (T)-GREENING THE WORLD AND FEEDING PEOPLE. (C) Anesa Co., Ltd

November 01, 2012

AYUBU RIOBA ALIPOTOA NONDO ZA NGUVU CHUO KIKUU CHA TAMPERE, FINLAND

AYUBU RIOBA akiwa katika Chuo Kikuu cha Tampere, jijini Tampere nchini Finland, ambako anapata Shahada ya Udaktari wa Falsafa(Phd) katika Sayansi ya jamii.
Kabla ya kufanikiwa kutunikiwa shahada hiyo, alitumia muda wake zaidi saa mbili(masaa mawili) kutetea utafiti wake juu ya "Media Accountability in Tanzania's Multiparty Democracy: Does Self Regulation Work"?
Baada ya mjadala mzito wa kitaaluma na maswali mengi kutoka kwa Profesa Audrey Gadzekpo kutoka Chuo Kikuu cha Accra, Ghana, pamoja na jopo la Maprofesa walifikia hitimisho na kumtunukia Shahda ya Falsafa ya uDAKTARI(Phd) katika fani ya Sayansi ya Jamii. Bila shaka ni jambo la kujivunia kwa watanzania na kwake AYUBU RIOBA. Mwenyzi Mungu ampe afya njema na kumlinda.

October 30, 2012

MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO SEKRETARIETI YA AJIRA NCHINI

MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO ULIOFANYIKA 27 OCT, 2012, DUCE-DAR ES SALAAMPDFPrintE-mail

Usaili wa Mahojiano kwa waliofaulu mtihani wa mchujo mkoa wa DAR ES SALAAM utafanyika tarehe 01/11/2012 na 02/11/2012 katika Ofisi za Sekretarieti ya Ajira zilizoko ghorofa ya pili jengo la Maktaba Kuu ya Taifa Barabara ya Bibi Titi Mohamed

EXAMINATION RESULTS FOR WARD EXECUTIVE OFFICER II-DSM
(ORAL INTERVIEW ON Thursday 01 November, 2012)   
   
SOMA ZAIDI MAJINA HAPA: