Showing posts with label Nyasa. Show all posts
Showing posts with label Nyasa. Show all posts

March 26, 2018

MWONEKANO WA ZIWA NYASA KATIKA KIJIJI CHA MBAHA WILAYA YA NYASA

March 22, 2018

CHANGAMAOTO YA WAKAZI WA MWAMBAO WA ZIWA NYASA NI BARABARA

February 23, 2018

KAMBALE SAMAKI WA AJABU KULIKO SAMAKI WOTE DUNIANI

NA JACOB MALIHOJA
 
NIMEFUATILIA kwa kina samaki wa aina tofauti wa ajabu kama vile Electrical El (Mwenye uwezo wa kuzalisha umeme hadi Volts 900 yaani mara nne ya umeme tunaoutumia majumbani), 

Ngisi mwenye uwezo wa kujibadili rangi kama kinyonga kulingana na mazingira anayokuwepo na mwenye nguvu kubwa za kung'ata kuliko nguvu za kung'ta za simba, au Nyangumi kwa ukubwa wake .. binafsi nampa namba moja Kambale baada ya kugundua ni samaki pengine yaweza kuwa kiumbe wa kwanza kuishi mahali kwa miezi au miaka bila kupata chakula.

MBOGA 7


Ukiwa mji kama wa Dar es salaam utasikia stori nyingi za Mboga 7. Au ukiwa maeneo ya mijini hii stori ya mboga 7 imezoeleka sana kusimuliwa. Lengo ni kuelezea familia yenye uwezo wa kuandaa mlo mmoja ukiwa umesheheni mboga za kila aina(nyingi). Lakini kwa wakazi wa Nyasa na Kijiji cha Lundu suala la Mboga 7 ni kawaida sana. Tofauti iliyopo ni kuelezea mazingira tu. Pengine watu wa mjini “Mnalamba lamba tu, hamshibi kisa hamna mboga”. Njoeni Lundu.

February 19, 2018

UHONDO WA NYASA NA VITOWEO VYAKE

WAKATI MWINGINE TUNATAFITI MAMBO MBALIMBALI KATIKA MWAMBAO WA ZIWA NYASA

Kizito Mpangala
Kizito
Honorius Mpangala

Bwana Kizito na Honorius Mpangala wakiwa kwenye msitu ya kando kando ya Mlima Chipyaghela ambao unaingia hadi ziwani. Ilikuwa kwenye shughuli za kuchunguza mapango yaliyotumiwa yaliyopo katika eneo la Tingitingi, ambayo mababu enzi hizo za vita kati ya wageni (wangoni) na wenyeji wa Kijiji cha Lundu.

MAMBA AKATISHA UHAI WA MJASIRIAMALI NGINDO

NA THOMAS CHIHONGAKI
Majonzi na Simanzi Vimetawala katika Kijiji cha Lundo na Ngindo Kata ya Lipingo kutokana na tukio la dada yetu Neema Kalanje(25) kupoteza maisha kwa kushikwa na kuuliwa katika Mto Lwika uliopo Kijiji cha Lundo. 

Dada yetu amekutwa na umauti huo jana Saa 5 Asubuhi akiwa katika shughuli zake za ujasiriamali wa kuuza Dagaa Nyasa aliowanunua Ziwani Asubuhi na kwenda kuwauza katika Kitongoji cha Zambia katika Kijiji cha Ngindo.

Marehemu alipofika katika Kivuko cha Mto Lwika kuna dalaja dogo la Mbao akaamua kunawa Maji ghafla mamba akatokea na Kumkamata. Baadae Taarifa zilisambaa kijijini  kwa mayowe na hatimaye Wananchi wakakusanyika na kuanza kutafuta na kufanikiwa kuuona mwili wa Marehemu.

Eneo hilo ni hatari kwani mwaka 2015 palitokea ajali na kujeruhiwa kwa kijana Ignas Magic Kalenyula na kumuua Thomas Nkoma. Rai yangu kwa Halmashauri kupitia Idara ya Maliasili kuangalia uwezekano wa kuwasaka wanyama hao na kuwatokomeza kabisa.

Pia Idara ya Ujenzi Nyasa kutusaidia kujenga daraja la kudumu katika eneo hilo. Picha za tukio nii kwa hisani ya C.Ngwata Diwani wa Kata ya Lipingo (Chadema). Natoa pole zangu kwa Familia ya akina Kalanje na Mdogo wangu Elisha Magunga kwa kumpoteza Mke wake Mpendwa...
RIP Neema

MWONEKANO WA BAADHI YA MAENEO YA ZIWA NYASA. KISIWA CHA NGINDO NA SHUGHULI ZA UVUAJI WA SAMAKI

 
PICHA; Kwa hisani ya Vitus Matembo, Mbamba Bay.

February 17, 2018

WIKIENDI NJEMA WASOMAJI WETU NA PICHA ZA MAENEO YA UZAMIAJI WA SAMAKI LUNDU, NYASA

Eneo hili ni miongoni mwa yanayotumiwa na wazamiaji wengi kupata samaki. Uzamiaji wa samaki katika eneo hili hutafutwa samaki wa mapambo. Kijiji cha Lundu hutumika sana kutafuta samaki wa mapambo. Kuna samaki wazuri mno wanaotafutwa hivyo wazamiaji hutegemea kijiji hiki kujipatia samaki hao.
Watoto wakioposha samakini karibu na jiwe Stima (Liganga Stima).

February 16, 2018

MBUFU NI AINA YA SAMAKI KUTOKA HAPA KWETU NYASA


Upikaji wa samaki hawa hauhitaji kitunguu wala nyanya au mafuta. Wanapikwa na kulika vizuri, hawahitaji mafuta ya kupikia, nyanya wala vitunguu na vikorombwezo vingine vya mapishi. Ukitumia viungo hivyo basi utakuwa umeharibu kabisa ladha yake na kupoteza asili yake. Ni samaki watamu mno.

February 10, 2018

MIAKA 72 NA UBORA WA WAHANDISI WA KIJERUMANI PAMOJA NA WAASHI WA TANGANYIKA KIJIJINI LUNDU

NA KIZITO MPANGALA
MIAKA 72 tangu jengo hili la kiroho liliponengwa halijaleta usumbufu kiujenzi. Msingi wake ni imara. Ni mwaka 2005 pekee jengo hili liliathiriwa na kimbunga (chinangunga) ambapo ni paa pekee liliharibiwa na ni sehemu ndogo sana iliyoathiriwa. Ilikarabatiwa kwa muda mfupi na kukamilika. Boriti zake kwenye paa hata watu 10 boriti moja hawawezi kunyanyua. Huu ni uhandisi wa Wajerumani.

Tazama upande wa juu kuna msitari mweusi umenyooka ukutani hapo. Hii siyo rangi kusema kwamba imepakwa. Hayo ni matofali yaliyoiva na kuzidi viwango vya ubora, na ni ngumu kwa matofali haya kuvunjika kirahisi. Hivyo msitari huo hapo juu ni urembo tu kiujenzi.

Kuni ambazo ni bora sana kuchomea matofali ni Miyombo. Miti hii ipo katika vinasaba vilivyopo kwenye makundi mawili. Kuna Myombo ambao mara nyingi huzalisha aina fulani ya kamba (mighoyi) ambazo zina matumizi makubwa sana katika jamii ya watu wa Nyasa. Aina ya pili ni Myombo unaoitwa "Mpangala", mti huu pia ni dawa nzuri sana endapo utasumbuliwa na tumbo hasa kwa wanaoharisha. Mimi ninatumia sana dawa hii pamoja na Mwarobaini.

February 05, 2018

MIONGONI MWA SAMAKI WANAOPATIKANA ZIWA NYASA

Mbelele
Kambale 
Magege

February 01, 2018

MARA PAAP! NAHODHA WA AZAM F.C ANAPOKUTANA NA MHARIRI MSAIDIZI WA BLOGU HII

Himid Mao akiwa na Kizito Mpangala

NGUVU YA MAWIMBI

UPANDE wa kushoto katika picha hii tazama jinsi mchanga ulivyojipanga. Haya ni matokeo ya vipindi mbalimbali katika Jiografia ya ziwa Nyasa. Kipo kipindi ambacho kikitokea mchanga huwa unasombwa na mawimbi na kupelekwa majini, hivyo unaweza kuingia majini na kutembea meta 50 na zaidi halafu kina si kirefu kwa sababu mchanga mwingi unakuwa umesambaa ndani ya maji. Kama unavyoona pichani, sehemu kubwa ya mchanga inemegwa. 

 Na kuna mchanga wenye rangi nyeusi inaying'ara nyakati za jua, pichani unaona sehemu fulani ya mchanga ni mweusi, ni mchanga unaovutia kwa macho.
Kipindi kingine ni kile kinachotokea halafu mchanga unarudishwa nchi kavu na kutengeneza kitu kama tuta fulani wakati huo ndani ya maji ukiingia unaweza kutembea meta 10 tu maji yakafikia shingoni, maana yake ni kwamba kina kinaongezeka kutokana na mchanga kurudi nchi kavu. 

January 27, 2018

MIONGONI MWA SAMAKI WANAOPATIKANA ZIWA NYASA

                           KARIBUNI NYASA

January 24, 2018

KITOWEO KATIKATI YA MANDHARI MAZURI NA YA KUVUTIA KATIKA UFUKWE WA NYASA

Dagaa Nyasa wakiwa wameandaliwa tayari kwa kuchomwa na kuandaa kitoweo.
Mandhari ya Nyasa
Mandhari ya maeneo ya kupumzika ufukweni

January 20, 2018

NDANI YA KISIWA CHA FALKLAND

NA ALBANO MIDELO, LITUHI
HIKI ni kisiwa kidogo cha Falkland ambacho kipo kwenye maingilio ya Mto Ruhuhu katika Ziwa Nyasa.Kisiwa hiki kinamilikiwa na wavuvi toka Ludewa mkoani Njombe na Nyasa mkoani Ruvuma.
Asili ya kisiwa hiki kuitwa Falkland ni mgogoro wa kugombania kisiwa hicho uliotokea mwaka 1982 kati ya wavuvi wa Ngelenge wilayani Ludewa wakati huo mkoa wa Iringa hivi sasa Mkoa wa Njombe na wavuvi wa Lituhi wakati huo wilaya ya Mbinga ambapo sasa ni wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma.

January 19, 2018

MTO MAKATA WASABABISHA USUMBUFU KWA VYOMBO VYA USAFIRI MBAMBA BAY

Tukiwa tunasubiri Ujenzi wa Barabara ya Mbinga-Mbambabay mwezi February 2018, hali ya barabara MTO Makata mjini Mbambabay leo si nzuri kwani imesababisha masuala ya usafiri kusimama kwa muda. 
Basi la Abiria likiwa limeshindwa kuendelea na safari kutokana na eneo la mto Makata kuwa bovu.
Picha kwa Hisani ya Egbert Jemeny(pichani).

January 18, 2018

HAPA NI UFUKWE WA CHIWINDI MPAKANI MWA TANZANIA NA MOZAMBIQUE.

Picha kwa hisani ya Egbert Jemeny

January 17, 2018

HALMASHAURI YA WILAYA YA NYASA INAO WAJIBU WA KUHUDUMIA BARABARA ZAKE

NYASA inahitaji matibabu kamili (kama dawa ya Mseto) sio kutuliza maumivu (Panadol). Matengenezo haya nimeyakuta mwezi Disemba 2017. Niliwaacha watengenezaji wakiwa kijiji cha Ndumbi, lakini yanaonekana yameanzia kijiji cha Amanimakolo (nako kunajazwa vifusi na kukarabati).
UJUMBE WANGU: Halmashauri ya Nyasa inao wajibu wa kuhudumia barabara zake wakati wote si kujaza vifusi kwakuwa Mheshimiwa Waziri Mkuu anapotembelea au kiongozi yeyote, au shughuli yoyote ya muda inapofanyika. Barabara ni nyenzo muhimu sana ya kukuza uchumi wa eneo lolote. Kila la heri wahusika. Tutaendelea kukumbushana.