Showing posts with label Nyasa. Show all posts
Showing posts with label Nyasa. Show all posts
March 26, 2018
MWONEKANO WA ZIWA NYASA KATIKA KIJIJI CHA MBAHA WILAYA YA NYASA
March 22, 2018
CHANGAMAOTO YA WAKAZI WA MWAMBAO WA ZIWA NYASA NI BARABARA
February 23, 2018
KAMBALE SAMAKI WA AJABU KULIKO SAMAKI WOTE DUNIANI
NA JACOB MALIHOJA
NIMEFUATILIA kwa kina samaki wa
aina tofauti wa ajabu kama vile Electrical El (Mwenye uwezo wa kuzalisha umeme
hadi Volts 900 yaani mara nne ya umeme tunaoutumia majumbani),
Ngisi mwenye uwezo wa
kujibadili rangi kama kinyonga kulingana na mazingira anayokuwepo na mwenye
nguvu kubwa za kung'ata kuliko nguvu za kung'ta za simba, au Nyangumi kwa
ukubwa wake .. binafsi nampa namba moja Kambale baada ya kugundua ni samaki
pengine yaweza kuwa kiumbe wa kwanza kuishi mahali kwa miezi au miaka bila
kupata chakula.
MBOGA 7
Ukiwa mji kama wa Dar es salaam
utasikia stori nyingi za Mboga 7. Au ukiwa maeneo ya mijini hii stori ya mboga
7 imezoeleka sana kusimuliwa. Lengo ni kuelezea familia yenye uwezo wa kuandaa
mlo mmoja ukiwa umesheheni mboga za kila aina(nyingi). Lakini kwa wakazi wa Nyasa na Kijiji
cha Lundu suala la Mboga 7 ni kawaida sana. Tofauti iliyopo ni kuelezea
mazingira tu. Pengine watu wa mjini “Mnalamba lamba tu, hamshibi kisa hamna
mboga”. Njoeni Lundu.
February 19, 2018
UHONDO WA NYASA NA VITOWEO VYAKE
WAKATI MWINGINE TUNATAFITI MAMBO MBALIMBALI KATIKA MWAMBAO WA ZIWA NYASA
![]() |
| Kizito Mpangala |
![]() |
| Kizito |
![]() |
| Honorius Mpangala |
Bwana Kizito na Honorius
Mpangala wakiwa kwenye msitu ya kando kando ya Mlima Chipyaghela ambao unaingia
hadi ziwani. Ilikuwa kwenye shughuli za kuchunguza mapango yaliyotumiwa
yaliyopo katika eneo la Tingitingi, ambayo mababu enzi hizo za vita kati ya
wageni (wangoni) na wenyeji wa Kijiji cha Lundu.
MAMBA AKATISHA UHAI WA MJASIRIAMALI NGINDO
NA THOMAS CHIHONGAKI
Marehemu alipofika katika Kivuko
cha Mto Lwika kuna dalaja dogo la Mbao akaamua kunawa Maji ghafla mamba
akatokea na Kumkamata. Baadae Taarifa zilisambaa kijijini kwa mayowe na hatimaye Wananchi wakakusanyika
na kuanza kutafuta na kufanikiwa kuuona mwili wa Marehemu.
Majonzi na Simanzi Vimetawala katika
Kijiji cha Lundo na Ngindo Kata ya Lipingo kutokana na tukio la dada yetu Neema
Kalanje(25) kupoteza maisha kwa kushikwa na kuuliwa katika Mto Lwika uliopo Kijiji
cha Lundo.
Dada yetu amekutwa na umauti
huo jana Saa 5 Asubuhi akiwa katika shughuli zake za ujasiriamali wa kuuza
Dagaa Nyasa aliowanunua Ziwani Asubuhi na kwenda kuwauza katika Kitongoji cha
Zambia katika Kijiji cha Ngindo.
Marehemu alipofika katika Kivuko
cha Mto Lwika kuna dalaja dogo la Mbao akaamua kunawa Maji ghafla mamba
akatokea na Kumkamata. Baadae Taarifa zilisambaa kijijini kwa mayowe na hatimaye Wananchi wakakusanyika
na kuanza kutafuta na kufanikiwa kuuona mwili wa Marehemu.
Eneo hilo ni hatari kwani mwaka
2015 palitokea ajali na kujeruhiwa kwa kijana Ignas Magic Kalenyula na kumuua
Thomas Nkoma. Rai yangu kwa Halmashauri kupitia Idara ya Maliasili kuangalia uwezekano
wa kuwasaka wanyama hao na kuwatokomeza kabisa.
Pia Idara ya Ujenzi Nyasa kutusaidia
kujenga daraja la kudumu katika eneo hilo. Picha za tukio nii kwa hisani ya C.Ngwata
Diwani wa Kata ya Lipingo (Chadema). Natoa pole zangu kwa Familia ya akina
Kalanje na Mdogo wangu Elisha Magunga kwa kumpoteza Mke wake Mpendwa...
RIP Neema
MWONEKANO WA BAADHI YA MAENEO YA ZIWA NYASA. KISIWA CHA NGINDO NA SHUGHULI ZA UVUAJI WA SAMAKI
February 17, 2018
WIKIENDI NJEMA WASOMAJI WETU NA PICHA ZA MAENEO YA UZAMIAJI WA SAMAKI LUNDU, NYASA
Eneo hili ni miongoni mwa yanayotumiwa na wazamiaji wengi
kupata samaki. Uzamiaji wa samaki katika eneo hili hutafutwa samaki wa mapambo. Kijiji cha Lundu hutumika sana kutafuta samaki wa mapambo. Kuna samaki wazuri mno wanaotafutwa hivyo wazamiaji hutegemea kijiji hiki kujipatia samaki hao.
![]() |
| Watoto wakioposha samakini karibu na jiwe Stima (Liganga Stima). |
February 16, 2018
MBUFU NI AINA YA SAMAKI KUTOKA HAPA KWETU NYASA
February 10, 2018
MIAKA 72 NA UBORA WA WAHANDISI WA KIJERUMANI PAMOJA NA WAASHI WA TANGANYIKA KIJIJINI LUNDU
NA KIZITO MPANGALA
MIAKA 72 tangu jengo hili la
kiroho liliponengwa halijaleta usumbufu kiujenzi. Msingi wake ni imara. Ni
mwaka 2005 pekee jengo hili liliathiriwa na kimbunga (chinangunga) ambapo ni
paa pekee liliharibiwa na ni sehemu ndogo sana iliyoathiriwa. Ilikarabatiwa kwa
muda mfupi na kukamilika. Boriti zake kwenye paa hata watu 10 boriti moja
hawawezi kunyanyua. Huu ni uhandisi wa Wajerumani.
Tazama upande wa juu kuna
msitari mweusi umenyooka ukutani hapo. Hii siyo rangi kusema kwamba imepakwa.
Hayo ni matofali yaliyoiva na kuzidi viwango vya ubora, na ni ngumu kwa
matofali haya kuvunjika kirahisi. Hivyo msitari huo hapo juu ni urembo tu
kiujenzi.
Kuni ambazo ni bora sana
kuchomea matofali ni Miyombo. Miti hii ipo katika vinasaba vilivyopo kwenye
makundi mawili. Kuna Myombo ambao mara nyingi huzalisha aina fulani ya kamba
(mighoyi) ambazo zina matumizi makubwa sana katika jamii ya watu wa Nyasa. Aina
ya pili ni Myombo unaoitwa "Mpangala", mti huu pia ni dawa nzuri sana
endapo utasumbuliwa na tumbo hasa kwa wanaoharisha. Mimi ninatumia sana dawa
hii pamoja na Mwarobaini.
February 05, 2018
MIONGONI MWA SAMAKI WANAOPATIKANA ZIWA NYASA
February 01, 2018
MARA PAAP! NAHODHA WA AZAM F.C ANAPOKUTANA NA MHARIRI MSAIDIZI WA BLOGU HII
NGUVU YA MAWIMBI
UPANDE wa kushoto katika picha hii tazama jinsi mchanga ulivyojipanga. Haya ni matokeo
ya vipindi mbalimbali katika Jiografia ya ziwa Nyasa. Kipo kipindi ambacho
kikitokea mchanga huwa unasombwa na mawimbi na kupelekwa majini, hivyo unaweza
kuingia majini na kutembea meta 50 na zaidi halafu kina si kirefu kwa sababu
mchanga mwingi unakuwa umesambaa ndani ya maji. Kama unavyoona pichani, sehemu
kubwa ya mchanga inemegwa.
Na
kuna mchanga wenye rangi nyeusi inaying'ara nyakati za jua, pichani unaona
sehemu fulani ya mchanga ni mweusi, ni mchanga unaovutia kwa macho.
Kipindi
kingine ni kile kinachotokea halafu mchanga unarudishwa nchi kavu na
kutengeneza kitu kama tuta fulani wakati huo ndani ya maji ukiingia unaweza
kutembea meta 10 tu maji yakafikia shingoni, maana yake ni kwamba kina
kinaongezeka kutokana na mchanga kurudi nchi kavu. January 27, 2018
MIONGONI MWA SAMAKI WANAOPATIKANA ZIWA NYASA
January 24, 2018
KITOWEO KATIKATI YA MANDHARI MAZURI NA YA KUVUTIA KATIKA UFUKWE WA NYASA
Madhumuni
kumbukumbu,
Nyasa,
Nyumbani
January 20, 2018
NDANI YA KISIWA CHA FALKLAND
NA ALBANO MIDELO, LITUHI
HIKI ni kisiwa kidogo cha
Falkland ambacho kipo kwenye maingilio ya Mto Ruhuhu katika Ziwa Nyasa.Kisiwa
hiki kinamilikiwa na wavuvi toka Ludewa mkoani Njombe na Nyasa mkoani Ruvuma.
Asili ya kisiwa hiki kuitwa
Falkland ni mgogoro wa kugombania kisiwa hicho uliotokea mwaka 1982 kati ya
wavuvi wa Ngelenge wilayani Ludewa wakati huo mkoa wa Iringa hivi sasa Mkoa wa
Njombe na wavuvi wa Lituhi wakati huo wilaya ya Mbinga ambapo sasa ni wilaya ya
Nyasa mkoani Ruvuma.
January 19, 2018
MTO MAKATA WASABABISHA USUMBUFU KWA VYOMBO VYA USAFIRI MBAMBA BAY
Tukiwa tunasubiri Ujenzi wa Barabara ya Mbinga-Mbambabay
mwezi February 2018, hali ya barabara MTO Makata mjini Mbambabay leo si nzuri
kwani imesababisha masuala ya usafiri kusimama kwa muda.
Basi la Abiria likiwa limeshindwa kuendelea na safari kutokana na eneo la mto Makata kuwa bovu.
Picha kwa Hisani ya Egbert Jemeny(pichani).
January 18, 2018
HAPA NI UFUKWE WA CHIWINDI MPAKANI MWA TANZANIA NA MOZAMBIQUE.
Picha kwa hisani ya Egbert Jemeny

Madhumuni
Nyasa
January 17, 2018
HALMASHAURI YA WILAYA YA NYASA INAO WAJIBU WA KUHUDUMIA BARABARA ZAKE
UJUMBE WANGU: Halmashauri ya
Nyasa inao wajibu wa kuhudumia barabara zake wakati wote si kujaza vifusi
kwakuwa Mheshimiwa Waziri Mkuu anapotembelea au kiongozi yeyote, au shughuli
yoyote ya muda inapofanyika. Barabara ni nyenzo muhimu sana ya kukuza uchumi wa
eneo lolote. Kila la heri wahusika. Tutaendelea kukumbushana.
Subscribe to:
Posts (Atom)




























