Showing posts with label kiswahili. Show all posts
Showing posts with label kiswahili. Show all posts

November 23, 2017

FREDDY MACHA ALIVYOLIZUNGUMZIA JUKWAA LA KISWAHILI SOCIETY

NA MARKUS MPANGALA 
SWALI: Naam, shikamoo Mzee Macha?
FREDDY MACHA; Marahaba. Habari zako bwana! uko wapi wewe siku hizi? Maana tangu tuliposalimiana pale Soma Café,Mikocheni na baadaye Nyumba ya Sanaa, Dar es Salaam wakati wa warsha nilizoendesha huko.
SWALI; Nipo hapa Bongo naendelea vema tu. Ni kweli, kitambo hatujawasiliana, pia nilifaidika sana na warsha zako hata hivyo si neno, tutaongea kidogo leo.
Freddy Macha
 FREDDY MACHA; Asante. Nadhani leo unalo la kuongea zaidi. Karibu.
SWALI; Ni kweli, nahitaji mengi kutoka kwako mzee wangu. Kiu yangu ni huu mradi wa Kiswahili Society, kwani umeeleza mahala fulani nikasoma nami nimevutiwa ili niwaarifu wasomaji. Je mradi huu ulianza lini na wapi?
FREDDY MACHA; Umeanzishwa na wanafunzi na Wahadhiri wa Kiswahili pale chuo cha lugha cha SOAS (School of Oriental and African Studies) hapa London,Uingereza.
SWALI: Nini dhumuni la kuanzishwa kwa Kiswahili Society?
FREDDY MACHA; Kuunganisha Wazungumzaji wa Kiswahili duniani lakini hasa hapa Uingereza.
SWALI: Nashukuru sana. Ndugu Macha, wewe ni Mwanamuziki,Mwanafasihi,na Mwandishi mkongwe. Katika fani hizi kuna mambo mengi umejifunza kutoka bara letu la Afrika,Latin Amerika,Marekani na sasa Ulaya. Unadhani jamii za watu wa Ulaya hususani Uingereza zinaweza kuhamasika kukiendeleza Kiswahili? 

November 20, 2017

KONGAMANO LA KUMBUKIZI YA FIDEL CASTRO


Jukwaa la Wajamaa Tanzania, Taasisi ya Usomaji na Maendeleo "Soma" na Rastafarai United Front wanashirikiana kuandaa kongamano la kumkumbuka El Commandante Fidel Castro siku ya Jumamosi, tarehe 25/11/2017. Mahala itakuwa kwenye ukumbi wa Soma Book Cafe; na muda ni saa 7 mchana hadi saa 12 jioni.
WOTE MNAKABISHWA. HAKUNA KIINGILIO!
"Mwambie Comrade amwambie Comrade"

November 02, 2017

KAMPUNI YA MKUKI NA NYOTA WAINGIA SOKO LA VITABU CHINA


NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM

KAMPUNI ya Mkuki na Nyota ambayo hujishughulisha na uchapaji wa vitabu imetanua wigo wa soko lake la uchapishaji na utangazaji wa vitabu baada ya kusaini makubaliano na Shirika la World Affairs Press (WAP) la nchini China.
 
Akizungumza baada ya kusaini makubaliano hayo Mkurugenzi wa MNN, Mkuki Bgoya amesema kuwa wamesaini Makubaliano na Shirika la World Affairs Press (WAP) ya China kufanya kazi pamoja katika miradi mbalimbali ya kuchapisha na kuvitangaza vitabu ikiwa ni njia mojawapo ya kutanua soko la kampuni hiyo barani Asia.

Mkuki na Nyota ni kampuni mashuhuri kwa uchapaji wa vitabu ambayo ilianzishwa mwaka 1992 jijini Dar es salaam. Mwanzilishi wa kampuni hiyo ni Walter Bgoya ambaye alitumia uzoefu wake wa miaka 18 ya kuwa Meneja Mkuu wa Tanzania Publishing House. 

December 22, 2012

PhD YA KWANZA KUANDIKWA KWA LUGHA YA KISWAHILI UDSM

Na Honorius Ngachipanda, Mbeya

Katika hali ambayo inaleta matumaini makubwa kwa wapenzi wa lugha ya Kiswahili, taarifa wkamba Dk. Metho Samweli amefanikiwa kuandika Thesis yake ya PhD ya somo la Kiswahili kwa lugha ya Kiswahili ni za kusisimua.
Kwa mujibu wa gazeti la THE HILL OBSERVER la Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Dk Method Samweli amekuwa mhitimu wa kwanza wa Chuo hicho kuandika Thesis ya PhD kwa lugha ya Kiswahili. The Hill Observer limeeeleza kuwa kwa muda mrefu sana wahitimu wote walikuwa wakiandika thesis zao lwa lugha ya kiingereza. 
Lakini Dk Method Samweli mwenye miaka 32 ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu kishiriki cha Elimu (UDSM-DUCE) ametunukiwa PhD hivi karibuni wakati wa sherehe za 42 zilizofanyika kwenye ukumbi wa MCCC (Mlimani City Conference Center).
Mkuu wa Idaya ta fasihi, Mawasiliano na Uchapishaji katika Idara ya Kiswahili ya Chuo kikuu cha Dar es salaam, Dk. Shani Omari alisema kuwa kabla ya thesis ya Dk method Samweli, hapakuwahi kutokea Thesis yoyote iliyoandikwa kwa lugha ya Kiswahili Chuoni hapo. 
Aidha, Chuo Kikuu cha Dar es salaam kinafuata nyayo za Chuo kikuu cha Dodoma (UDOM) ambacho tayari wapo wanafunzi kadhaa walioandika thesis zao lugha ya Kiswahili. Miongoni mwa wahitimu wa PhD waliofanikiwa kuandika Thesis zao kwa lugha ya kiswahili, ni Mohamed Seif Khatibu ambaye ni waziri mwandamizi na kiongozi wa siku nyingi ndani ya CCM.

WASIFU WA DK. METHOD SAMWELI
Alijiunga sekondari ya Ndanda, kisha akajiunga na UDSM mwaka 2002 hadi mwaka 2006 alipomaliza masomo yake ya B.A with Education na kuwa mhadhiri msaidizi wa UDSM-DUCE. Kati ya mwaka 2006 na 2008 alimaliza masters katika masomo ya Linguistic hapo hapo UDSM.