Showing posts with label amani na upendo. Show all posts
Showing posts with label amani na upendo. Show all posts

March 07, 2018

JOSEPH BOIMANDA: MTAJI WA MILIONI HAMSINI SERIKALI HAWANA MUDA WA KUKUFUATILIA

NA.HONORIUS MPANGALA
MAISHA popote unaweza kusema hivyo kwani waliofikiria katika hoja hii walikuwa na sababu za msingi zilizokuwa na maana kiuhalisia. Wakati kipato ndio sababu hasa zilizopelekea kukawa na maneno kama haya ambayo yanasadifu uhalisia wa maisha. Katika mazungumzo yangu na mmoja ya watanzania waishio nchini Afrika kusini ilinifanya nistaajabu kile anachonieleza ambacho ndio uhalisisa wa maisha ya huko.

Ni rafiki yangu na ndugu yangu Joseph Boimanda alinifanya nistaajabu pale aliposema mtaji wa milioni hamsini za kitanzania ukiwa Afrika Kusini sio lolote kwa serikali ya huko. Maisha yamekuwa yenye uhuru na amani ya kutosha kwa raia.
Wakati nataka kuyajua haya ananieleza kuwa mamlaka ya mapato ya huko haina muda wa kufuatilia mfanyabiashara wa kati.Kama inatokea mtu anataka kulipa mapato serikalini basi ni hiari yake,hii ni kwa wale wafanyabiashara wadogo na wa kati amabao mtaji yao ni kitu kidigo kwa serikali yao. 

February 16, 2018

MBUFU NI AINA YA SAMAKI KUTOKA HAPA KWETU NYASA


Upikaji wa samaki hawa hauhitaji kitunguu wala nyanya au mafuta. Wanapikwa na kulika vizuri, hawahitaji mafuta ya kupikia, nyanya wala vitunguu na vikorombwezo vingine vya mapishi. Ukitumia viungo hivyo basi utakuwa umeharibu kabisa ladha yake na kupoteza asili yake. Ni samaki watamu mno.

November 24, 2017

JIWE LA POMONDA NA FORODHANI PANAWEZA KUTUPATIA WATU WA 'DIVING' KATIKA MASHINDANO YA OLIMPIKI.

NA HONORIUS MPANGALA

LICHA ya kuwa mazingira mazuri na yenye kila aina ya vivutio lakini wafrika tunashindwa kuwa wabunifu wa katika kuyafanya kama fursa.Mungu aliiumba Afrika hivi ilivyo na kuweka jiografia ambayo nyakati zote watu Wa mataifa ya ulaya wamekuwa wakivutiwa nayo.
Mmmoja wa Warukaji katika Jiwe la Pomonda, Ziwa Nyasa
Iko michezo mingi inayochezwa Ulaya na Amerika inatokana na jinsi wenzetu walivyo makini katika kutumia mazingira yao katika kujipatia fursa ya maisha yao. Nyakati zote mataifa ya wazungu yamekuwa na michezo mingi ambayo ina mashabiki na wanafanya vyema,hakuna michezo ambao unakosa mashabiki Amerika na Ulaya.

November 13, 2017

KWANINI SEKRETARIETI YA AJIRA HAINA MATAWI NCHINI?

NA MARKUS MPANGALA
MIAKA kadhaa iliyopita nilishindwa kuwaelewa kabisa watendaji wa Wakala  wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) hapa nchini. Nilikuwa siwaelewi kwa sababu siku moja niliwahushudia wafanyabiashara fulani kutoka Songea mkoani Ruvuma, wakizunguka vyumba vya ofisi vya taasisi hiyo kwenye jengo la Ushirika liliko Barabara ya Lumumba, Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam kwa madhumuni ya kusajili kampuni yao.  
Jenista Mhagama

Pili,niliwahi kumsaidia rafiki yangu, Albert Nyaluke Sanga, ambaye ni mfanyabiashara mkubwa mkoani Iringa, ili apate leseni ya biashara. Haikuwa leseni yake binafsi, bali aliamua kumsaidia kijana mmoja aliyekuwa na ndoto za kuwa mfanyabiashara, lakini alikosa pa kunzia.
Rafiki yangu huyo anapenda kuwasaidia vijana wanaojishughulisha na ujasiriamali kwa sababu anaamini hiyo ndiyo njia pekee ya kuwakomboa, badala ya elimu yao na kuondokana na matembezi ya kusambaza bahasha za kuomba nafasi za kazi.

November 04, 2017

UTALII: UFUKWE WA KIJIJI CHA LUNDU

Wilaya ya Nyasa imebarikiwa kuwa na fukwa zuri zinazotokana na ziwa Nyasa. Huu mojawapo ya ufukwe wenye historia kubwa sana, kupokea wageni kutoka Ujerumani, Uingereza, Italia na nchi mbalimbali ambao wengi wao walikuja kupitia Shirika la Benedictine Fathers la Peramiho na wengine kwa njia zao binafsi. Ni ufukwe wenye kumbukumbu nzuri sana kwa wakazi na wageni.
KARIBUNI NYASA.

November 03, 2017

UCHAMBUZI WA KITABU: IT CAN'T BE TRUE



KITABU: IT CAN’T BE TRUE
MWANDISHI: JOHN MWAKYUSA
MCHAMBUZI: MARKUS MPANGALA

HII ni mara yangu ya kwanza kusoma riwaya ya mwandishi John R.P. Mwakyusa, mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam. Riwaya inaitwa “It Can’t Be True: A Story from Uganda-the Pearl of Africa”, na kuchapishwa kwa mara ya kwanza mwaka 2017 na kampuni ya Partridge Publishing ya India.

October 21, 2017

TABASAMU NA KITABU


Ragin Mmbanga (kushoto) na Markus Mpangala (Kulia)
Huyu ni rafiki yangu. Anaitwa Ragin Mbaga, ila tuwapo farashani hupendelea kumwita "Mzee wa bustani ya usomaji". 

October 17, 2017

UTAMU WA WIMBO WA TAIFA UKO KOMBE LA DUNIA.

NA. HONORIUS MPANGALA
 
ILIKUWA miaka Sita ya Ubabe wa soka barani Afrika kuanzia mwaka 2006 hadi 2012. Kila mpenzi wa soka alimfahamu Hassan Shehata,kila mpenzi wa soka alimfahamu Waile Gomaa. Ilikuwa nyakati za Misri kunyanyasa mataifa mengine ndani ya bara la Afrika. Ilimchukua Kameruni miaka tisa kulipiza manyanyaso aliyopata toka kwa Misri ya kiumeni mwaka 2008 pale Ghana.
Ni Misri ambayo iliipa hasara CAF kuunda kombe lingine la Afcon baada ya kulibeba lile awali Mara nne Mfululizo. Mwaka 2006 fainali zilizoandaliwa na Misri wakikutana na Ivory coast ya Didier Drogba.
KIKOSI CHA MISRI

Fainali ile iliisha kwa matuta na wenyeji kutwa taji. Licha ya kuwa na kikosi ambacho kilikuwa na vijana taklibani Saba wakitoka kikosi cha Al Ahly ambayo ilikuwa moto wa kuotea mbali. Hapa nawazungumzia Mohammed Barakat,Saeed Moward,Essam El Hadary,Ahmed Hassan,Hossam Hassan,Mohammad Mido,Mohammed Aboutrika na wengineo. Ilikuwa ni kikosi kilichojaa vipaji kikiwa na hamasa kubwa kutoka kwa kocha mzawa Hassan Shehata kiliwafanya wapinzani wafikirie Mara mbili zaidi.

October 02, 2017

UTALII KATIKA WILAYA YA NYASA

Makala haya yalichapishwa kwneye gazeti la HABARI LEO kuelekea suala la utalii katika wilaya ya Nyasa.

September 29, 2014

UJENZI WA SOKO KUU NYASA

SOKO KUU LA WILAYA YA NYASA KATIKA HATUA ZA MWISHO KUKAMILIKA.

December 22, 2013

UHABA WA SAMAKI



Mwandishi wetu Vitus Matembo amezoea kula samaki huko Nyasa, lakini kwa sasa analalamika kuwa kuna uhaba wa Samaki. Katika hali ya kawaida miezi ya Septemba, Oktoba mpaka Novemba kunakuwa na uhaba wa samaki wa aina fulani. Kwa wanyasa kuna samaki wanawapenda sana, lakini wanapotoweka basi inakuwa tatizo. 

Hivyo kwa sasa samaki wanaopatikana zaidi ni maarufu kama MCHUKWA, lakini samaki aina ya Kambale upatikanaji wake ni mgumu kipindi hiki labda kuanzia januari. Na kwakuwa wanyasa wamezoea kula samaki wanono basi tusmishangae ndugu yetu Matmebo akilalamikia kukosekana kwa samaki anaowapenda.
Ndiyo Nyasa yetu, raha na changamoto.
Kwa sasa ununuzi wa Kambale unaweza kuuziwa kipande badala ya kambale mzima. Hapo ni kipande cha Kambale akiwa tayari kwa kuuzwa. KARIBUNI NYASA


February 04, 2013

CHOMBEZO: WEKA MALENGO MAISHANI

Markus Mpangala

Ni mwenyezi Mungu anayetuweka hai kwenye hii dunia huku wenyewe tukichukua jukumu la kujilinda dhidi ya hatari zozote. Leo ninapenda kukuelezea jambo lililonishangaza zaidi ingawaje nilikwisha simuliwa nyakati fulani na baadhi ya wanazuoni, na lenye elimu muwali. Jambo hili ndilo linalenga kukuuliza maswali haya; wewe ni mfanyakazi kwenye ofisi fulani, hivi unafanya kazi ili iweje? Labda wewe huna kazi, unaishi ili iweje? Kwanini huna kazi au shughuli yoyote? Lau umri wako mdogo au hujapata kazi, unadhani kuna umuhimu wa kazi? Na kwanini unaona kuna umuhimu wa kuishi kama ulivyo? Wengine ni wafanyabiashara na mengineyo; hivi katika maisha yako una malengo gani? Yaani unaamka mapema, unakwenda kazini aidha kwa usafiri wako au wa jamii (Daladala).
Unakwenda ofisini kufanya nini? Lengo lako hasa ni nini kadiri mshale wa saa unavyokwenda hapa duniani? Unaishi ili kufanya nini? Kwanini unadhani una haki ya kuishi na si yule au mimi? Lengo lako la kuishi liko wapi? Sababu yako ya kufanya kazi iko wapi? Ndiyo, unapenda cheo, halafu iweje? Ukishakupata cheo hicho unalengo gani na maisha yako?
Unadhani cheo chako kitaisaidia nini ofisi yako? Kwanini wewe unapenda sana kupendelewa? Unapotaka kupendelewa je, wewe umewafanyia upendeleo wenzako? Unadhani ukipendelewa wewe ni muhimu kuliko yule na mimi? Lengo lako la kupendelewa ni nini? Unapenda kupewa kuliko wewe kutoa? Lengo lako ni nini hasa?

Jiulize sana msomaji ili tuende sambamba nikupe jambo hili. Tueleweshane hapa kwamba kuna umuhimu mkubwa sana wa kuweka malengo katika maisha yetu haya. Kama wewe huna ndoto basi hutafanikiwa. Kama wewe huna maono maishani, basi una kazi kubwa kujitambua. Una kazi kubwa ya kutambua uendako. Ni lazima uanze kufikiri sasa, maana mtu mwerevu huzifikiria hatua zake. Basi tusiende mbali msomaji mpenzi, nakupenda sana, tambua hilo.
Shaban akitimiza majukumu yenye malengo ofisini kwake
Sikiliza sasa, Aprili 19 mwaka huu nilinunua kitabu cha “Barrack Obama: Yes, We Can”, kimeandikwa na Lila Luce. Mambo yaliyomo kitabuni ndiyo yananifanya nitafakari nawe leo kupitia safu hii. Rudi juu anza kusoma upya halafu uelewe zaidi. Kwenye kitabu hiki kuna mambo ambayo sikujua kuhusu Rais huyu wa Marekani. Inachekesha na kuelimisha, lakini ukweli maisha aliyopitia Barrack Hussein Obama (jina lake la utani Barry O’Bomber) kuna mengi ya kujifunza.
Ukisema mitishamba, Obama amenyweshwa sana kule Kogelo, Kenya. Ukisema Daladala, basi Obama amepanda sana pale Kenya (huita Matatu). Obama alikuwa mtumiaji wa madawa ya kulevya (teja) enzi za ujana wake, tafakari hilo.

Obama ana kauli mbiu ya “Mabadiliko”. Mabadiliko ni dhana ambayo ilitokana na aliyoona na kuishi maishani mfano Kogelo na Indonesia. Tusione Obama anaongoza Marekani, alilumbana na mkewe (Michelle Obama) kwa wazo la Urais. Michelle akamwita msaliti, hamwelewi anafikiria nini juu ya familia, alimwambia; “mume wangu nitawezaje kulea mabinti hawa wawili (Natasha na Malia) peke yangu?

Lakini Obama alimjibu mkewe, “tafadhali hii ni mara yangu ya mwisho, kabla ya kuishi kwa utulivu mke wangu, niruhusu.” Msomaji unapaswa kutambua kuwa wakati anagombea kuwa Useneta alitofautiana na mkewe, lakini aliruhusiwa kwa ahadi hatawania kiti kingine.
Obama anakufunza mengi; alifundishwa imani ya Ukristu na akawa mkristu, akajifunza Uislamu alipokuwa Indonesia, kwahiyo dini zote kazipitia kabla ya kufunga pingu za maisha kwa Mchungaji Jeremiah Wright. Alifundishwa mila na desturia za Wamasai. Alishatumia Vibatari kule Kogelo, Kenya. Alitembea kwa miguu vijijini, hakika ni mengi mno. Hata hivyo kauli aliyomwambia mkewe wakati anaomba amruhusu kuwani Urais ndiyo inatuleta hapa leo msomaji.

Awali alisema, ‘Nimeona nafasi ya kushinda’. Hii ilitokana na malengo yake aliyoweka ili kutimiza ndoto zake. Akamjibu mkewe, ‘hii ni nafasi ya mwisho mke wangu. Nahitaji kuyafanyia kazi mawazo yangu kabla sijatulia na kuishi kwa amani kwenye familia yetu.”  
Hii inakuonyesha ndoto zake maishani. Inakuonyesha malengo yake maishani. Inakupa mwanga wa kutengeneza sura mpya na kuacha ya kale. Inakupa matumaini mapya ambayo lazima utayatendee kazi.
Rafiki yangu Shaban a.k.a Don King, akiwa ofisini kwake
Lazima uwe na malengo maishani msomaji. Ujue dhumuni lako maishani. Tambua hakuna aliyeandikiwa kufanikiwa au kupewa uhalali wa kukusanya mafanikio yote. Hayupo binadamu aliyeshushiwa mafanikio kutoka mbinguni bila kuweka mkazo kwenye malengo yake. Anza kutimiza ndoto zako kwa kuweka malengo yafanyayo kazi. Amini juhudi zako na mawazo yako ni muhimu mno kwa jamii. 
Jamii inahitaji mawazo yako ambayo unatakiwa kuyatendea kazi. Fanya kazi kwa bidii ukiwa unajua dhumuni lako ni lipi. Tumia kipato chako kwa uangalifu maana huwezi kujenga nyumba ukiwa mwingi wa starehe. Wapo wajinga wachache hawaweki akiba na kila kukicha wanalalamika maisha magumu. Ndugu yangu kama huna malengo maishani ni bure. Utaishi kulingana na mazoea tu yaliyomo.
Unakwenda kazini, mwisho wa mwezi ukifika mshahara wote unalipa madeni. Halafu eti unataka kulingana na tajiri wa Mexico Carlos Slim au Tokyo Sakswalle wa Afrika Kusini. Mafanikio hutengenezwa, katu mafanikio hayakutengezi wewe. Ukitaka kufanikiwa lazima ujue njia zake halali na kubuni mpya ambazo zitakupa sura mpya ya maisha yako. Ndoto zako zitakupa msukumo wa kufanikiwa.
Anza sasa kupanga vipaumbele. Pima kipato chako kama kinakuruhusu kufanya yanayokuzidi. Mawazo yako mazuri yakuongoze ili ufanikiwe. Tumia 80% kufuatilia fursa zilizopo na mpya.

January 15, 2013

MRADI WA MAJI KIJIJI CHA NG'OMBO WAKAMILIKA

Na Mwandishi  wetu, Ng'ombo
Wakazi zaidi ya 2450 wa kijiji cha Ng’ombo katika Kata ya Chiwanda wilayani Nyasa mkoani Ruvuma wameondokana na adha iliyokuwa ikiwakabili ya upatikanaji wa maji safi na salama baada ya kukamilika kwa ujenzi wa mradi wa maji kijijini hapo,

Akizungumza na Lundunyasa Network, Mhandisi wa Maji wa Wilaya hiyo Amos Mtweve alisema mradi huo ambao umejengwa kwa ufadhili wa UNDP kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira umegharimu jumla ya shilingi 298,346,700 na kwamba kuna vituo 23 ambavyo wakazi wa kijiji hicho watakuwa wakivitumia kupata maji.
Mhandisi Mtweve alisema kuwa kabla ya kujengwa kwa mradi huo wananchi walikuwa wakilazimika kutumia maji ya ziwa Nyasa kwa ajili ya kunywa, kupikia, na kuoga hali ambayo ilikuwa ikihatarisha usalama wa afya zao.
Alisema pamoja na changamoto mbalimbali zilizokuwa zikijitokeza wakati wote wa ujenzi wa mradi huo ikiwemo baadhi ya wananchi kutojitokeza kuchangia nguvu zao kama uchimbaji wa mtaro kwa ajili ya kulaza mabomba lakini bado mradi umekamilika kwa kwango kilichotakiwa.
“kukamilika kwa mradi huu kimsingi ni sifa kubwa kwetu kwani itawapa matumaini wafadhili wetu kufadhili miradi mingine hasa ikizingatiwa kuwa UNDP wamefadhili miradi michache ya maji hapa nchini ikiwemo huu wa kwetu,” alisema Mhandisi Amos Mtweve.

December 29, 2012

'KUMRUDISHA MWAFRIKA KWENYE ASILI YAKE: MRADI MGUMU KULIKO YOTE"

Mimi na mzee Kamara Kusupa, hii leo Ofisini, mambo ya kuhariri kitabu chake kipya.

Kwa muda mrefu tumeshuhudia maandiko mengi kuhusiana na sisi waafrika. Yapo maandishi kama ya akina Cheikh Anta Diop, Dk. Elly Kamugisha, Franz Fanon, Julius Nyerere, Leopold Senghor na wengineo. Lakini jambo kubwa lililokuwa likijadiliwa ni nani hasa huyu MWAFRIKA. Mathalani wengi wanakubaliana kwamba mwafrika ni mtu mweusi, hivyo kuwatenga waarabu, wahindi, wazungu na wabarbaig ambao kimsingi nao wamejikuta wakiwa wamezaliwa katika bara ya Afrika. Msomi Dk Harrith Ghassany yeye alihoji nini asili ya Afrika na akaelezea kuwa ni kutoka kule Tunisia.
Dk Harrith alisema hayo kwenye kitabu chake cha KWAHERI UHURU, KWAHERI UKOLONI: ZANZIBAR NA MAPINDUZI YA AFRABIA. Ni moja ya changamoto alizotoa ambao kila mwenye udadisi atajikuta akishughulisha ubongo wake. Wapo wachambuzi makini kama Joseph Mihangwa ambaye kwa sasa maandiko yake yanapatikana katika gazeti la RAIA MWEMA, amekuwa akihojia mara kwa mara juu ya asili ya afrika na kuelezea mambo kadhaa yaliyowahi kutokea huko nyuma. Yote haya yanatuletea swali la msingi MWAFRIKA huyu ni nani?
Hata hivyo dunia imebadilika sana na kila kona inatusaidia kujua nini hasa kinachopaswa kusemwa kwa dhati na moyo safi kwa nyakati za sasa. Kuna wazungu wamezaliwa Afrika Kusini, Tanzania na wengine nchi nyingine za Afrika. Je hawa watakwenda wapi ikiwa hawajui asili zao zilikuwa namna gani. Ni kama ambavyo Waafrika wanavyojiuliza ni namna gani wataweza kurudi Afrika ambako hawajui waanzie wapi.

Ni vigumu leo kumwelezea Cliford Harris au T.I arudi afrika kutoka Marekani. Ni vigumu vilevile kumweleza Lennox Lewis arudi barani afrika. Ni vigumu kumwambia Danny Jordan wa Afrika Kusini kwamba uchotara wake sio kitu arudi kwenye asili ya makaburu. Au ni vigumu kumwambia Hellen Zille mwenyekiti wa chama cha upinzani cha D.A pale Afrika Kusini na gavana wa jimbo la Cape Town, kwamba arudi kwa wazungu wenzake. Hii ni moja ya mabadiliko makubwa ya mipaka ya nchi ambayo imeshindwa kuzuia mahusiano ya wanadamu kutoka nchi moja hadi nyingine au kutoka jamii ya nchi moja kwenda jamii ya nchi nyingine. Leo mwafrika anaweza kuzaa na mchina au Mkorea hivyo ni vigumu mtoto atakayezaliwa kutotambuliwa kuwa mwafrika, na kuangalia asili. 
Lakini wapo watu wanaojaribu kujiuliza ni namna gani wanaweza kuwakumbusha waafrika wenzeo kuwa Mwafrika alikuwa na asili yake. Ni mwafrika alikuwa wa kwanza kuwasilia Marekani kabla ya christopher Columbus, ambapo ushahidi mwingine uliandikwa na Profesa Ivan Sertima kwenye kitabu chake "THEY CAME BEFORE COLUMBUS". 
Nikiwa na mzee Kusupa. Duh anahamu mpaka amevunja meza.
Hata ukisoma 'voyage' mbalimbali za Columbus kumejaa mengi ya kushangaza na kwanini yanachukuliwa kuwa kama yalivyo?. Tukiacha hilo tunajikuta tunaangalia sisi Waafrika ni nani na asili yetu ikoje. Dhana ya uhai inakuwa kubwa na inachukua mkondo mkubwa sana, hivyo basi kitabu cha KUMRUDISHA MWAFRIKA KWENYE ASILI YAKE; MRADI MGUMU KULIKO YOTE hakika kinakuletea baadhi ya majibu ya maswali ambayo kila mara watu wanajiuliza. 
Hii inaonekana kuanzia kwenye DINI, SIASA, UTAMADUNI, na mengine mengi kuhusu Afrika yetu. Mwandishi wa kitabu hicho MWINJILISTI KAMARA KUSUPA anatuelezea mengi kwamba kuna makosa kadhaa yanafanyika, na amekuwa akisogea mbele kidogo zaidi ya anapoishia mwanazuoni kama Ali Mazrui. 
Kila jamii imekuwa kwenye asili yake, na inakuwa vigumu kurudi kwenye asili yake. Nini ambacho Kamara Kusupa anatuelezea kwenye kitabu hicho, hakika tunapaswa kuwa watulivu na kuvuta subira kwamba ni moja ya kitabu chenye mafunzo mengi kwa watu wa Afrika. Je, dini za waafrika ni zipi? Mfumo wa utawala wa waafrika ni upi? Msingi wao na dhana ya uhai vikoje? Uhusiano wao na jamii za nje ukoje? Je, mwafrika ataepuka dhahama ya mabadiliko ya kijamii duniani? Je, mwafrika ataweza kurudi katika asili yake? 
Nadhani ni moja ya mambo ya kusisimua na hakika yatakuwa na hamasa kwa wasomi na wananchi wengine. Ikumbukwe hicho kitakuwa kitabu cha tatu kutoka kwake, kwani alishaandika vitabu viwili; MAISHA YANGU GEREZANI, na kingine HII NDIYO TANZANIA TUNAYOITAKA. Kitabu cha pili nilishiriki kwa kiasi kikubwa, na sasa nashiriki pia kuhariri na kuweka lugha bora yenye hadhi kwa wasomaji makini. Ninadhani wasomaji watafurahia zaidi. Na tuseme basi kama kweli tutaweza kurudi kwenye asili yetu au ni mradi mgumu?    MWINJILISTI KAMARA KUSUPA atatujibu hilo, usikose kukisoma kitabu hicho.

December 27, 2012

MIKONO NA MOYO WA NATHAN MPANGALA KUWAFANYA WATOTO WENYE SARATANI KUTABASAMU

Nathan Mpangala akiwa anawafundisha watoto kuchora michoro mbalimbali. 
Nathan Mpangala ni miongoni mwa watanzania wanaogusa mioyo ya watu kutokana na kazi zao za sanaa. Wengi wanakumbuka michoro ya katuni za Kijastibikozi na mingine mingi sana. 
Yeye ndiye mwasisi wa michoro ya katuni za Daladala ambazo huchapishw ana gazeti la MAJIRA hapa nchini. Tasnia ya uchoraji imemfikisha katika nchi mbalimbali kuhudhuria mihadhara ya kuelimisha jamii akiwa miongoni mwa waandishi wa habari wanaotumia vipaji vyao kufikisha ujumbe kwa njia ya sanaa za michoro. Moja ya kazi zake kubwa zinazoonekana kote nchini kupitia Televisheni ya ITV ni kibonzo cha MTU KWAO. 
Kibonzo hivyo hubeba ujumbe mbalimbali wenye nia ya kuelimisha na kuburudisha jamii. Kutokana na kipaji chake, Nathan Mpangala anarudisha faida anayopata kwa kazi hiyo kwenda kwa jamii. 
Amekuwa akifanya hivyo kupitia programu ya WAFANYE WATABASAMU akiwa na lengo la kuwaliwaza watoto wote wanaougua saratani nchini. Juhudi hizo ni kutokana na mapenzi yake kwa jamii na nchi kwa ujumla. Kama anavyoonekana pichani akiwa na watoto hao, pamoja na mchoro mwingine upande wa kulia unavyoonyesha watu wasiofikiria jamii yao. 
Hakika Mikono na moyo wa NATHAN MPANGALA umekuwa faraja kwa wazazi wa watoto na watoto hao kwa ujumla. Nawe waweza kuchangia juhudi zake kwa kuungana naye katika WAFANYE WATABASAMU.


Anaelezea zaidi safari yake .............
UCHORAJI UMEPAMBA MOTO. Baadhi ya watoto wanaendelea na matibabu ya saratani katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, jijini Dar es Salaam, wakijimwayamwaya wakati wakichora. Kupitia Program ya Wafanye Watabasamu, nilitembelea watoto hao kuwapa zawadi kisha kuchora nao. 
Katika ziara hiyo niliyoambatana na baadhi ya wachoraji katuni na marafiki wa Wafanye Watabasamu tuliwazawadia watoto zawadi kisha kuchora nao. Kwa niaba ya watoto, nawashukuru ndugu na marafiki wa Programu ya Wafanye Watabasabu kwa zawadi mbalimbali walizochangia ambazo zimefanya ziara hiyo kuwa ya mafanikio. Pia nawashukuru sana marafiki na wachoraji wote waliojitokeza na kuungana nami Muhimbili. Picha na michoro mbalimbali iliyochorwa na watoto hayo iko njiani.

December 19, 2012

HALI YA WAVUVI NA UVUVI KATIKA ZIWA NYASA WILAYANI NYASA

Mvuvi akiwa na zana zake za kazi. 
PICHA: kwa hisani ya kaka Francis Godwin

UHABA wa samaki ziwa Nyasa upande wa Tanzania unaochangiwa na vifaa duni vya uvuvi umepelekea baadhi ya wanaume wa tarafa ya Mwambao wilaya ya Ludewa mkoani Iringa kutelekeza familia na kwenda nchini Malawi kufanya shughuli za uvuvi kama njia ya kukwepa changamoto za uchumi zinazoendelea kuwa kikwazo katika wilaya hiyo.
Uchumi wa wananchi wa tarafa yaMwambao ambao ulikuwa ukitokana na ajira ya uvuvi kwenye ziwa Nyasa nao umezidi kuporomoka kwa kasi kubwa na kupelekea hata biashara za wananchi wa maeneo hayo ambazo zilianzishwa kutokana na wingi wa wageni waliokuwa wakifika kujumua samaki kwenye ziwa hilo pia kuathirika kwa kiasi kikubwa.
Kama inavyofahamika kuwa uvuvi wa samaki kwa wananchi wa tarafa ya Mwambao wilayani Ludewa ndio shughuli kubwa ya kiuchumi ambayo imekuwa ikitegemewa na karibu robo tatu ya wakazi wa tarafa hii ya Mwambao na ndio shughuli iliyopelekea tarafa hiyo kuwa na mzunguko mkubwa wa fedha hasa kipindi cha nyuma japo kwa sasa imeanza kubaki historia pekee. 
Bonyeza kiungo;    SOMA ZAIDI HAPA

November 28, 2012

WARAKA KUTOKA MJINI LAHTI NCHINI FINALND


Na JACKLINE MLUGE-AUTIO, LAHTI-FINLAND

Wakati wote tunafikiria kuwa wenzetu wazungu wanapesa nyingi sana na ndio maana wanatusaidia. Lakini ukweli si kama wanapesa ila wana moyo wakufanya hivyo, ninasababu za kusema hivyo kwa sababu roho inaniuma kuona kuwa kuna baadhi ya watu ambao huwatesa watoto bila sababu ya msingi. Kila kukicha ukisoma katika magazeti mbalimbali ya Tanzania utakuta habari mbalimbali ambazo zinahusiana na kuteswa kwa watoto. Swali najiuliza kama kweli unamchukua mtoto wa mwezango kwa lengo la kumsaidia iweje leo umtese.
Kuna wangapi ambao wana moyo wa kuwatunza watoto wa wenzaao bila kuwatesa ni wakati umefika sasa Watanzania kuweza kubadilika ikiwa una mchukua mtoto wa mwenzako kwa lengo la kumtunza basi mtunze kweli na sivinginenvyo. Kuna usemi usemao kutoa ni moyo na si utajiri. Seija Saarikoksi Silvola ambaye ni  mama mwenye umri wa miaka 65 amebahatika kupata mtoto mmoja.
Jackline Mluge-Autio, akiwa na Mama Seija Saarikoksi nchini Finland.

Unaweza kujiuliza kwanini nimeamua kuandika makala hii? Nimeandika kwa nia ya kutoa changamoto kwa watanzania wenzangu kuweza kusaidia watu wengine hata kama tuna watoto zetu lakini pia kama unauwezo wa kusaidia inabidi tuweze kusaidia. Mara ya kwanza Seija, kufika bara la Afrika aliposhinda zawadi ya tiketi ya kwenda nchi ya kama unavyojua kwa mara ya kwanza kufika Afrika aliweza kuvutiwa na ukarimu wa watu ambao kwa nchi kama ya Finland ukarimu ni kitu kigumu sana.
Jackline Mluge-Autio akiwa na rafiki zake.
Mwaka 2007 alienda Tanzania na shirika la Settlement na baadhi ya wafini ambao walienda kutengeneza shule ya msingi Pekomisegese iliyopo mkoa wa Morogoro. Nakumbuka mwaka huo, mimi nilikuwapo ingawa sikuweza kukaa kwa muda mrefu kutokana na masomo. Tulikuwa tunalala kwenye mahema. Wafini walikuwa wanafanya kazi kwa kushirikiana na wakazi wa Pekomisegese. Na weza kutoa pongezi zangu na shukrani zangu kwa wakazi hao wa Pekomisegese kwani waliweza kushirikiana kwa hali na mali kwa kujitolea kuweza kujenga shule ambayo leo hii watoto wanaweza kukaa darasani na kujisomea.
Jackline akiwa na wanafunzi wenzake.
Mwaka 2009-2010 Seija na baadhi ya wafini walienda kujitolea kujenga shule ya msingi Pinda iliyopo Mgeta mkoa wa Morogoro. 2011-2012 shule ya msingi Tandale. Mbali na kujitolea kujenga shule pia Seija ana watoto zaidi ya kumi ambao anawasidia kwa hela yake mwenyewe bila kutegemea NGO. Ana wasidia kwa kuwalipia ada za shule na kuwanunulia vifaa vya shule. Sio kwamba eti Seija ni tajiri , la hasha ni ana moyo. Ikiwa mtu kutoka mbali anaweza kutusaidia je sisi wenyewe tunashindwa najua kabisa kuna mashirika ambayo yanasaidia watoto lakini pia mtu mmoja mmoja tunaweza kujitolea na kuwasaidia watoto wetu wa tanzania wenzetu bila kujali kabila au dini.  Kumsaidia mtu si mpaka umjue.