Showing posts with label uzuri. Show all posts
Showing posts with label uzuri. Show all posts

February 23, 2018

MBOGA 7


Ukiwa mji kama wa Dar es salaam utasikia stori nyingi za Mboga 7. Au ukiwa maeneo ya mijini hii stori ya mboga 7 imezoeleka sana kusimuliwa. Lengo ni kuelezea familia yenye uwezo wa kuandaa mlo mmoja ukiwa umesheheni mboga za kila aina(nyingi). Lakini kwa wakazi wa Nyasa na Kijiji cha Lundu suala la Mboga 7 ni kawaida sana. Tofauti iliyopo ni kuelezea mazingira tu. Pengine watu wa mjini “Mnalamba lamba tu, hamshibi kisa hamna mboga”. Njoeni Lundu.

February 17, 2018

WIKIENDI NJEMA WASOMAJI WETU NA PICHA ZA MAENEO YA UZAMIAJI WA SAMAKI LUNDU, NYASA

Eneo hili ni miongoni mwa yanayotumiwa na wazamiaji wengi kupata samaki. Uzamiaji wa samaki katika eneo hili hutafutwa samaki wa mapambo. Kijiji cha Lundu hutumika sana kutafuta samaki wa mapambo. Kuna samaki wazuri mno wanaotafutwa hivyo wazamiaji hutegemea kijiji hiki kujipatia samaki hao.
Watoto wakioposha samakini karibu na jiwe Stima (Liganga Stima).

February 16, 2018

MBUFU NI AINA YA SAMAKI KUTOKA HAPA KWETU NYASA


Upikaji wa samaki hawa hauhitaji kitunguu wala nyanya au mafuta. Wanapikwa na kulika vizuri, hawahitaji mafuta ya kupikia, nyanya wala vitunguu na vikorombwezo vingine vya mapishi. Ukitumia viungo hivyo basi utakuwa umeharibu kabisa ladha yake na kupoteza asili yake. Ni samaki watamu mno.

February 05, 2018

MIONGONI MWA SAMAKI WANAOPATIKANA ZIWA NYASA

Mbelele
Kambale 
Magege

January 27, 2018

MIONGONI MWA SAMAKI WANAOPATIKANA ZIWA NYASA

                           KARIBUNI NYASA

December 27, 2017

NI NYASA PEKEE HUPATIKANA AINA HII YA SAMAKI KATIKA DUNIA HII


SAMAKI ZIWA NYASA

Inakadiriwa kuna aina 700-1000 ya Samaki wa aina ya Cichlids katika Ziwa Nyasa. Samaki hao hawapatikani sehemu zingine duniani isipokuwa Ziwa Nyasa (Endemic). Samaki hao hutafutwa sana na wageni ambao hutengeneza MatankiMaji ya vioo kwaajili ya maonyesho (Aquarium).

MUHIMU; Pichani ni ufukwe wa Lundu upande wa kaskazini-magharibi unaitwa "Bandarini". Ni sehemu iliyokuwa inatumiwa na meli za MV. Iringa na MV.Songea kutia nanga. Katika ratiba iliyopo Meli mpya za mizigo ya MV.Ruvuma na MV Njombe hazitatia nanga hapa kwetu.

Lundu, Nyasa
Disemba 22/2017.

SALAMU KUTOKA LUNDU, ZIWA NYASA

Nawasalimu enyi waungwana nikiwa nimeketi katika ngazi za Kanisa Katoliki ambalo lilijengwa mwaka 1946 ikiwa ni mwaka mmoja baada ya kumalizwa vita vya dunia. Mahali hapa nilipatiwa daraja la Kipaimara.
Kinachoshangaza jengo hili limekuwa imara maradufu. Jengo hili halina mambo yenu ya #ExpansionJoints. Jengo la Kanisa hili lilijengwa na waafrika wakisimamiwa na Wamisionari wa Shirika la Benedictine Fathers la Kijerumani. Kwa mujibu wa historia rasmi iliyohifadhiwa hapa matofali ya jengo hili yalifyatulia kijiji cha Liweta na Lundu kutokana na udongo mzuri. Aidha, matofali hayo yalisafirishwa kwa Boti ya Stella Maris. 

Wasalaamu!
"Bruda" Markus Mpangala OSB
Lundu, Nyasa.
Disemba 20/2017.

MUHIMU; Salamu hizi ziliandikwa kabla ya tarehe ya leo.

December 11, 2017

WAZIRI MKUU ATAMBUE NYASA IMEJAA UTAJIRI-2

Na MARKUS MPANGALA
SEHEMU ya kwanza ya makala haya katika safu hii tulichagiza kuwa agizo lililotolewa na Waziri mkuu katika hotuba yake akimwagiza Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamis Kigwangala kuanzisha Mamlaka ya Fukwe za Bahari na Maziwa ili kutangaza utalii na kuendeleza fukwe ambazo hazina shughuli kwa madhumuni ya kukuza utalii Kanda ya Kusini na mengineyo. Endelea kusoma….

Madhali linalozungumzwa ni kuhakikisha fukwe zinakuwa na tija ni muhimu pia kuikumbusha mamlaka husika kuwa wilaya ya Nyasa inao utajiri mkubwa sana wenye tija kupitia sekta ya utalii ambayo kihistoria maeneo mengi bado ni mbegu bora n zenye kuvutia. 

Si hilo, wilaya hiyo inao uwezo wa kuwa na viwanda vya uzalishaji wa bidhaa mbalimbali lakini kwa sharti moja muhimu; iwapo changamoto zinazoikabili Halmashauri zitattuliwa kwani zitakuwa chachu ya kukuza mapato ya ndani. Hatuimwagii sifa hizo za bure bali yapo mambo ya kuyaangalia kwa kina. Leo ninatoa mifano mingine ambayo kwa namna moja au nyingine itawafumbua macho wasomaji na watu mbalimbali wanaofuatilia mfululizo huu. 

FUKWE
Sifa kubwa ya Ziwa Nyasa ni kuwa fukwe bora na zisizo na uchafu wowote. Kama tulivyoona wiki iliyopita sifa zilizotajwa na rafiki yangu Ilan kutoka Israel, ndivyo ukweli ulivyo. Katika Kijiji cha Mtupale kilichopo Kata ya Chiwanda kuna fukwe za mawe ambazo ni kivutio adimu cha utalii. Ukitembelea mwambao mwa ziwa Nyasa kuna maeneo mengi yenye fukwe za mchanga unaovutia, lakini katika mwambao mwa Kata ya Chiwanda kuna fukwe za mawe ambazo bado wawekezaji hawajafungua milango ya Utalii kanda ya Kusini. 
Ufukwe wa Mchanga katika forodha ya Chivanga iliyopo kijijiji cha Lundu



Ikumbukwe Kijiji hicho kinapakana na kingine cha Chiwindi ambacho ndicho cha mwisho kabla ya kuingia mpaka kati ya Tanzania na Msumbiji. Eneo hili linao ubora wa hali ya juu. Zipo fukwe zingine zenye kuwavutia watu ni Ndengere, Ngindo, Lundo, Lipingo, Mkali, Hongi,Liuli,Kihagara,Mkili, Lundu,Mbaha, na Ndumbi kwa kuzitaja chache ni sehemu ambazo zinahitaji nguvu kidogo sana za uwekezaji kabla ya kuleta tija kwa wawekezaji. Ikumbukwe kijiji cha Ndumbi ndicho chenye bandari ambayo Makaa ya Mawe yanayochimbwa na Kampuni ya TanCoal. Ni mahali ambapo unaweza kutumia darubini kuitazama nchi jirani ya Malawi kwa ufasaha. 

December 09, 2017

SALAMU KUTOKA LUNDU, ZIWA NYASA

Nipo kijijini kwetu Lundu kwa muda wa mwezi mmoja sasa. Naendelea kukusanya taarifa mbalimbali zinazofaa kuchapishwa hapa barazani “Karibuni Nyasa”.  Kama tunavyoona habari mbalimbali za utalii, basi ndivyo utakavyosikia habari usizowahi kuzijua kutoka mwambao wa Ziwa Nyasa. Mazingira yanayovutia mno, yenye kuhitaji kutembelewa.
 
Kuna picha mbili; ya kwanza nikiwa katika Mto Chipapa, uliopo mtaa wa Likwambe hapa hapa kijijini Lundu. Ni mto ambao miaka 1990 ulikuwa ukitiririsha maji yake mwaka mzima kwa ufasaha. Lakini sasa mambo yamebadiliika, hakuna uwezekano huo. Kwahiyo mto huo unangojea msimu wa masika kama hivi sasa uweze kuwa na maji ya kutiririsha hadi Ziwa Nyasa.

November 30, 2017

KITOWEO NA MANDHARI YA KUVUTIA YA LIULI, NYASA


Picha ya kwanza (juu) inaonyesha utulivu wa Ziwa Nyasa katika bandari ya Liuli, wilayani Nyasa.  Ikumbukwe Ziwa Nyasa linasifika kwa mawimbi makali lakini pia linakuwa na utulivu kama huu pichani. 

Picha ya Pili (chini) inaonyesha samaki aina ya Mbufu ambao wamekuwa wakipataikana kwa wingi katika ZIwa hilo. Samaki hao huvuliwa maeneo mengi zaidi ya mwambano wa Ziwa Nyasa. Ni miongoni mwa kitoweo kinachopendwa zaidi na wenyeji  na wageni.

November 24, 2017

JIWE LA POMONDA NA FORODHANI PANAWEZA KUTUPATIA WATU WA 'DIVING' KATIKA MASHINDANO YA OLIMPIKI.

NA HONORIUS MPANGALA

LICHA ya kuwa mazingira mazuri na yenye kila aina ya vivutio lakini wafrika tunashindwa kuwa wabunifu wa katika kuyafanya kama fursa.Mungu aliiumba Afrika hivi ilivyo na kuweka jiografia ambayo nyakati zote watu Wa mataifa ya ulaya wamekuwa wakivutiwa nayo.
Mmmoja wa Warukaji katika Jiwe la Pomonda, Ziwa Nyasa
Iko michezo mingi inayochezwa Ulaya na Amerika inatokana na jinsi wenzetu walivyo makini katika kutumia mazingira yao katika kujipatia fursa ya maisha yao. Nyakati zote mataifa ya wazungu yamekuwa na michezo mingi ambayo ina mashabiki na wanafanya vyema,hakuna michezo ambao unakosa mashabiki Amerika na Ulaya.

November 22, 2017

FUKWE ZA LUNDU, KARIBUNI ZIWA NYASA

 Hapa ni Forodha ya Lundu. Eneo hili lina fukwe mzuri sana kama huu. Picha ya Juu ni upande wa Kusini mwa forodha. Picha ya chini ni upande wa kaskazini magharibi mwa forodha hiyo. Ufukwe huu umepokea wageni kutoka Ujerumani, Italia, na wengineo ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Karibuni sana Lundu. Karibuni Wilaya ya Nyasa.

October 21, 2017

TABASAMU NA KITABU


Ragin Mmbanga (kushoto) na Markus Mpangala (Kulia)
Huyu ni rafiki yangu. Anaitwa Ragin Mbaga, ila tuwapo farashani hupendelea kumwita "Mzee wa bustani ya usomaji". 

October 05, 2017

DAR ES SALAAM TANZANIA