Showing posts with label mbamba bay. Show all posts
Showing posts with label mbamba bay. Show all posts

January 05, 2018

UZINDUZI WA MELI MPYA YA MV. RUVUMA KWA WILAYA YA NYASA ULIOFANYIKA LEO MJINI MBAMBA BAY

MV Ruvuma ikiwa imetia Nanga katika Bandari ya Mbamba Bay
Mbunge wa Jimbo la Nyasa na Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Stella Manyanya (wa pili kutoka kushoto) akitoka kukagua meli hiyo.
Mmmoja wa Manahodha wa MV Ruvuma akisalimia na viongozi wa Chama cha Mapinduzi na Serikali bandarini Mbamba Bay.
Mv. Ruvuma

January 04, 2018

SALAMU KUTOKA MBAMBA BAY, ZIWA NYASA

Honorius Mpangala
..Niko Mbamba Bay katika Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa hususani Idara ya Elimu. Kuna changamoto ambayo wanaipata wakazi wa Wilaya ya Nyasa, nawashangaa sana wale wanaosema kuna usawa wa utoaji wa huduma kati ya Mikoa na Wilaya. Hii keki haigawiwi sawa.

Miundombinu ya Barabara mibovu, eneo la mlima wa Malongo, Kata ya Kihagara ni korofi na sumbufu miaka nenda rudi. Ukifika baadhi ya maeneo ya kijiji cha Chinula ukorofi wa mlima Malongo nao uko vilevile. Mvua ikinyesha tu ni shida hata pikipiki kupandisha mlima haiwezekani. Utelezi uko eneo kubwa sana la Mlima Malongo na kijiji cha Chinula.

December 27, 2017

NYASA; DISEMBA 20 ILIPONIREJESHA MIAKA 13 ILIYOPITA

NA HONORIUS MPANGALA, LUNDU
TULIANZA safari yetu na dadangu kijijini kwetu Lundu na kuelekea Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa Mbamba Bay. Changamoto za barabarani hazikukosa kwasababu ya mvua zinazonyesha. Tukifika na kukamilisha yaliyotupeleka huko. 

Saa kumi jioni nilipofika kituo cha mabasi cha Mbamba Bay sikukuta gari ya kugeuza kwenda kwetu Lundu. Ikatulazimu tupande ya kuishi njiani, gari iliyotoka Mbinga kwenda Kihagara. Nikiwa nawaza namna ya kutoka Kihagara hadi Lundu lakini nikapanga jambo kuwa bodaboda ziko kila eneo sikuhizi,na sikutoa nauli ya yangu na Dada nikamwambia waambie natoa Mimi. Nikamwambia konda natoa Kihagara kuna mtu anatusubiri,nilifanya Kwa maksudi.

December 04, 2017

BANDARI YA MBAMBABAY ITAKUZA UCHUMI

NA MWANDISHI WETU, SONGEA

NAIBU Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhandisi Stella Mànyanya ameshauri kupanuliwa kwa bandari ya Mbamba Bay iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa Mkoa wa Ruvuma ili kufungua milango ya uwekezaji katika ukanda wa kusini.



November 22, 2017

MAONI YA MHARIRI: ‘Nani atalinda samaki wa Ziwa Nyasa?


Naanza katika maliasili zetu. Sisi kama Tanzania tuna maliasili nyingi sana na watu wengi hawajui kabisa hilo na pia tuna wataalamu wangeweza kuwafumbua watu macho. Tukianza kwa kusafirisha nje ya nchi, Samaki hai wa maji baridi yaani Tanzania ndio ina samaki wa bei kubwa kuliko wote duniani. 

November 16, 2017

MBAMBA HILL KUWA HIFADHI YA PILI YA ASILI TANZANIA KUWA MJINI

NA MWANDISHI WETU 
MKOA wa Ruvuma unatarajia kupata hifadhi ya wanyamapori ya pili ya asili inayoitwa Kilima Mbamba (Mbamba Hill) ambayo ipo mjini Mbamba Bay makao makuu ya wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma. 
Hifadhi pekee Tanzania ya kwanza ya asili iliyopo mjini inaitwa Luhira iliyopo kilometa saba toka mjini Songea mkoani Ruvuma iliyoanzishwa mwaka 1974. Mkoa wa Ruvuma unapata hifadhi ya pili ya asili mjini. 

MV NJOMBE INAVYOFUNGUA FURSA KWA WAKAZI ZIWA NYASA.


Honorius Mpangala, 0628994409

NA. HONORIUS MPANGALA
AKIWA katika kampeni za urais mwaka 2005 Rais mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete katika ardhi ya Kyela Mkoani Mbeya alihaidi meli. Alirudia tena kauli hiyo alipokuwa katika ardhi ya Mbamba Bay Mkoani Ruvuma. Baada ya kipindi cha utawala wake hatimaye meli alizoahidi tayari zimeonwa na Wanyasa. 

MV Njombe imekamilika na kufanikiwa safari moja ya majaribio kutoka Bandari ya Itungi hadi Mbamba Bay.  Yapo mambo ambayo ni fursa kwa wakazi wa Nyasa kutokana Meli hii. Kama inavyoitwa ni meli ya mizigo ni chombo kitakachoweza kuwainua kiuchumi wakaza wa Nyasa kama watakitumika ipasavyo. Kuinuka kiuchumi kutatokana na kujikita katika shughuli ambazo wakazi wake watajishughulisha na shughuli kama ilivyo kilimo biashara na hata ufugaji wa kisasa na wenye tija katika maisha ya leo.
Kilimo cha biashara ni moja ya ujasiriamali ambao watu wengi wamekuwa wakijishughulisha nao. Katika mwambao wa Ziwa Nyasa hususani wilaya Nyasa yapo mabonde ambayo yanaweza kufanyika kilimo cha mazao ya muda mfupi na kwa mfumo wa kilimo cha umwagiliaji, na kile cha kutegema mvua na kuleta tija.


November 15, 2017

KISIWA CHA MBAMBA BAY KIMEPENDEKEZWA KUWA HIFADHI

NYUMA yangu ni kisiwa cha Mbambabay wengine wanakiita kisiwa cha Zambia kilichopo Mbamba Bay wilayani Nyasa mkoani Ruvuma ambacho kimependekezwa kuwa Hifadhi ya wanyamapori. Kisiwa hicho kina ukubwa wa hekta 27.kisiwa hicho kimejaliwa kuwa na uoto unaovutia wa misitu ya miombo ambao ni maarufu duniani ambapo mawe yanayozunguka katika kisiwa hicho ni mazalia ya samaki wa mapambano aina zaidi ya 400 wanaopatikana katika ziwa Nyasa pekee.
Kutokana na udogo wa kisiwa cha Mbambabay Afisa Maliasili na Utalii wa Mkoa wa Ruvuma Afrikanus Challe anashauri katika kisiwa hicho kusijengwe makazi ya kudumu kwa ajili ya wafanyakazi wa kuhudumia watalii ili kuendelea kutunza uoto wa asili uliopo hivi sasa.
Albano Midelo

November 09, 2017

WILAYA YA NYASA INAO UTAJIRI WA VIVUTIO VYA UTALII

Mwonekano wa fukwe za Ziwa Nyasa.

October 27, 2017

KWANINI WILAYA YA NYASA IMESHIKA MKIA KATIKA MATOKEO YA DARASA LA SABA?



RAYMOND NDOMBA, SONGEA
WILAYA ya Nyasa iliyopo mkoa wa Ruvuma imekuwa ya mwisho katika matokeo ya darasa la saba mwaka huu 2017 kimkoa. Swali la kujiuliza ni kwanini hali hiyo imetokea. 


Mawazo yangu ni haya; Pamoja na sababu nyingi zilizosababisha matokeo hayo ya aibu kubwa. Wazazi wanapaswa kubeba lawama kubwa. Wengi wao hawafuatilii maendeleo ya watoto wao, pia makuzi na malezi mabaya.

Miaka ya hivi karibuni (kuanzia mwaka 2000), Wazazi wengi katika wilaya ya Nyasa hawajali elimu, hawajigusi katika ufuatiliaji wa watoto wao kielimu na hata kitabia (Angalia matokeo ya mitihani ya Taifa ya shule za msingi na sekondari kunzia miaka hiyo ya 2000 kwa shule kongwe ndani ya wilaya). 

October 17, 2017

TAKWIMU MUHIMU ZA WILAYA YA NYASA HADI OKTOBA 2017


1. Total Number of Hamlets in the District = 425

2. Total Number of Households for Nyasa dc = 31,146

3. Total Female Population for Nyasa dc = 74,768.


4.Total Male Population for Nyasa dc = 71,392.

5. Total Population for Nyasa dc = 146,160.

6. Total Number of Secondary school = 14

7. Total Number of Primary School = 106
Total Number of Villages = 84


8. Total Number of Ward = 20

9. Total Number of Division = 3

CHANZO: Nyasa dc statistics

September 16, 2017

MBAMBA BAY HIGH SCHOOL

NA VITUS MATEMBO, MBAMBA BAY
KWA muda mrefu Wilaya ya Nyasa haikuwa na Shule ya sekondari yenye kidato cha tano na Sita. Wanafunzi na wazazi walilazimika kutumia gharama zao kutafuta shule za sekondari binafsi nje ya Wilaya hiyo. Kma inavyofahamika Wilaya ya Nyasa bado ni changa, hivyo inakabiliwa na changamoto ya shule za sekondari binafsi, kutokana na watu kutowekeza kwa kiwango cha juu.

Kutokana na hali hiyo sasa Ujenzi wa Shule ya sekondari ya Kidato cha tano na sita unaendelea mjini Mbamba Bay. Ni mojawapo ya hatua za nzuri za maendeleo. Shule hiyo ni ile iliyopo katika kijiji cha Ndengele kilichopo katika Kata ya Mbamba Bay.

Ujenzi unaendelea, shule hiyo itakuwa na jengo la ghorofa moja.
  
Baadhi ya majngo ya shule hiyo.


Mandhari ya shule hiyo.
  
Ujenzi unaendelea katika shule hiyo kuonmgeza madarasa kwa mtindo wa ghorofa ili kuwezesha kuchukua wanafunzi wengi kulingana na mahitaji na kupatiwa elimu.
PICHA ZOTE; VITUS MATEMBO.

June 27, 2014

NGUZO ZA UMEME ZAPELEKWA NYASA



Na Egbart Jeremy,Mbamba Bay
 
Hatimaye shehena ya kwanza ya Nguzo za Umeme iliwasilishwa Juni 20 mjini Mbambabay ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa kusambaza umeme vijijini pamoja na wilaya Nyasa ambayo ni mpya.

Kwa mujibu wa msimamizi wa mradi huo, Bwana Hugo alisema kuwa licha ya ubovu wa barabara lakini walifanikwia kuwasilisha shehena hiyo.

Alisema kuwa gari lilikuwa linakwama mara kwa mara ana kutokana na vifusi vilivyowekwa ikiwa ni jitihada kubwa zilizofanywa na Mbunge, John Komba kuwasiliana na maofisa wa TANROD mkoa wa Ruvuma wamwamuru mkandarasi kusambaza vifusi.

Kwa mujibu wa msimamizi wa mradi huo, alisema juhudi za kupeleka umeme wilaya ya Nyasa zimetokana na na  mbunge huyo. Mradi huo ulitakiwa kuanzia wilaya ya Tunduru lakini Mbunge Komba amejenga hoja hadi mpango ukabadilishwa kuanzia wilaya ya Nyasa

February 23, 2014

'BAY LIVE SOCIAL HALL' NA MASWALI KIBAO KWA WANYASA




Na Vitus Matembo, Mbamba Bay
 
Huu ni mwanzo tu wa hatua kufikia kilele. Ndugu yetu Madenge Chindogo kaanza hivi. Je wengine tunasubiri nini, mnawekeza tu mijini eeh!. Pengezo nyingi sana ndugu yetu huyu.
MAPROFESA 27; Wilaya ya Nyasa lakini Elimu Nyasa ni ya Mwisho. Kilosa na Chiulu ndio kumejaa maprofesa ila elimu yake majanga tu.

JAJI mstaafu B. Samatha tutakulilia sana ila Wanyasa hawatakusahau.
MJOMBA wangu wa damu, Luteni Jenerali C.L.MAKAKALA unacheo kikubwa sana. Tubebe ndugu zako wakinyasa hata Jeshini tu. Ndengele wanakulilia ulete maendeleo.

IGNATIO L. MATIMBA KOMBA, toka Tumbi. Nakuomba uje uwekeze Nyasa kielimu. Naheshimu sana nafasi yako ya ukaguzi kanda ya Kaskazini.
Kaka HOOPS KAMANGA, Rudi nyumbani uinue KILIMO Nyasa.
Mama STELLA MANYANYA kumbe ni mnyasa, usikusahau Nyasa.
HEBU TAJA WENGINE WENGI NA UELEZE NINI WAKIFANYE NYASA!!