Na.
HONORIUS MPANGALA
Nilikuwa
nchini Jamhuri ya kidemokrasi ya Kongo April 4, 2015 siku ya pasaka. Kulikuwa
na mchezo wa wa mtoano kuelekea kwenye makundi klabu bingwa Afrika kati ya Tp
Mazembe wenyeji dhidi ya Orlando Pirates. Mitaani kila uliyemwona alikuwa
amevalia jezi ya Mazembe na akizungumza kuhusu Mazembe huku wakielekea uwanjani
Estadio de Mazembe.
Nilimuuliza
mlinzi wa eneo nilioenda kuhusu mashabiki FC Lupopo hawawezi kwenda uwanjani?
Akanijibu hata Mimi ni Lupopo lakini inapokuja uwakilishi wote tunakuwa wamoja.
Akanieleza hata uwanjani huioni jezi ya Lupopo. Mechi ile ilimalizika kwa TP
kupata matokeo ya goli tatu kwa moja yaliyofungwa na Ranford Kalaba,Mbwana
Samata na Rogers Asale.
![]() |
| SIMBA |
Nilikaa
na mlinzi yule tukisikiliza matangazo ya redio kwa lugha ya kifaransa naye
alinitafsiria kwa kiswahili cha kikongo. Wakati magoli yote yanaingia katika
lango la Orlando alikuwa akisimama na kushangilia. Huo ndio utofauti wetu na
wao inapokuja suala la michuano ya kimataifa.
Sababu
ya pili ambayo inapelekea timu zetu za kitanzania kuwa na wakati mgumu ni kwa
upande wa wachezaji. Upande Huu unatokana na ile hali ambayo wachezaji
wanaichukulia katika mchezo. Huweza kuingia uwanjani wakiwa wamejiamini sana
lakini ni kelele za dakika chache toka kwa mashabiki wanao wafahamu zitawafanya
wachanganyikiwe.












