Showing posts with label soka. Show all posts
Showing posts with label soka. Show all posts

March 26, 2018

SIMBA, YANGA WANAIMBA KIMUNGU WANACHEZA KISHETANI.

Na. HONORIUS MPANGALA 
Nilikuwa nchini Jamhuri ya kidemokrasi ya Kongo April 4, 2015 siku ya pasaka. Kulikuwa na mchezo wa wa mtoano kuelekea kwenye makundi klabu bingwa Afrika kati ya Tp Mazembe wenyeji dhidi ya Orlando Pirates. Mitaani kila uliyemwona alikuwa amevalia jezi ya Mazembe na akizungumza kuhusu Mazembe huku wakielekea uwanjani Estadio de Mazembe. 

Nilimuuliza mlinzi wa eneo nilioenda kuhusu mashabiki FC Lupopo hawawezi kwenda uwanjani? Akanijibu hata Mimi ni Lupopo lakini inapokuja uwakilishi wote tunakuwa wamoja. Akanieleza hata uwanjani huioni jezi ya Lupopo. Mechi ile ilimalizika kwa TP kupata matokeo ya goli tatu kwa moja yaliyofungwa na Ranford Kalaba,Mbwana Samata na Rogers Asale. 
SIMBA

Nilikaa na mlinzi yule tukisikiliza matangazo ya redio kwa lugha ya kifaransa naye alinitafsiria kwa kiswahili cha kikongo. Wakati magoli yote yanaingia katika lango la Orlando alikuwa akisimama na kushangilia. Huo ndio utofauti wetu na wao inapokuja suala la michuano ya kimataifa.
Sababu ya pili ambayo inapelekea timu zetu za kitanzania kuwa na wakati mgumu ni kwa upande wa wachezaji. Upande Huu unatokana na ile hali ambayo wachezaji wanaichukulia katika mchezo. Huweza kuingia uwanjani wakiwa wamejiamini sana lakini ni kelele za dakika chache toka kwa mashabiki wanao wafahamu zitawafanya wachanganyikiwe.

March 02, 2018

MO IBRAHIM,INUKA JIPUKUTE VUMBI UENDE

Na.Honorius Mpangala
MABADILIKO ya bechi la ufundi katika klabu yoyote huja na matokeo chanya na hasi kulingana na mwenendo wa timu au klabu kwa ujumla.Katika hilo kuna mambo huenda yakawa tofauti kwa wachezaji walioonekana kupata sana nafasi kabla ya mabadiliko.Unayakumbuka maisha ya mchezaji wa Chelsea John Mikel Obi baaada ya kutumuliwa kwa Jose Mourinho pale klabuni.Ujio wa Guus Hindik ulirudisha kwenye hali ya kupata nafasi hadi kufikia hatua ya mashabiki wa kitazania walimpachika jina la Ombeni Sefue.

Kupachikwa kwa jina la Ombeni Sefue kwa Obi kulitokana na jinsi alivyoonekana kutotumika wakati wa Mourinhona alipofika Hidink akaanza kumpa nafasi.Hii ilifananishwa na Sefue wakati wa utawala wa awamu ya tano alivyokuwa hasikiki katika serikali hadi ilipoingia serikali ya awamu ya tano.


Mabadiliko ya makocha yanakuwa yenye kuleta mabadiliko katika vikosi kutokana na kila kocha hupenda kuja na falsafa zao.Hili ndilp lililomkumba mchezaji fundi wa mpira aliyepita katika mashamba ya miwa pale Manungu Turiani Mohammed Ibrahim.Hadi klabu ya Simba inafikia hatua ya kukubali uwezo wake na kumsajili ni kutokana na kile alichokuwa akikifanya akiwa na klabu ya Mtibwa Sugar.

Simba waliamua kufanya usajil ulijumuisha wachezaji watatu kwa pamoja toka Mtibwa sugar yaani waliwasajili Mzamiru Yassin,Shiza Kichuya nay eye Mo Ibrahim ambao walikuwa mhimili mkubwa wa klabu hiyo yeneye maskani yake katika mashamba ya miwa Manungu Turiani.

February 14, 2018

AFCON 2019: TUSIJISAHAU MWAKANI SIYO MBALI.

NA SAMWEL CHITANYA.
 
MWAKA 2017 utabaki kuwa mwaka unaokumbukwa na Watanzania wapenda soka. Mwaka huo ni mwaka ambao timu yetu ya vijana Serengeti Boys ilishiriki kwa Mara ya kwanza mashindano ya vijana kwa Afrika tangu Tanzania iwepo. Ushiriki huo ulikuja baada ya miaka 37 tangu Tanzania iliposhiriki kwa Mara ya kwanza fainali za kombe la Mataifa ya Afrika maarufu kama AFCON mnamo mwaka 1980.
Kikosi cha Serengeti Boys
Ilkuwa ni Furaha kubwa sana kuwaona vijana wa Serengeti Boys wakiwa wanashindana na timu kama Mali,Niger, Congo na timu nyinginezo zilizoshiriki mashinano Yale. Ingawa hatukufanya vema sana lakini angalau nasi tulionekana kama tunaweza. Nani alikuwa hafurahii kumuona Ramadhan Kabwili akiwa langoni na wenzie kama akina Ally Nganzi, Nasho Naftari, Nickson kibabage, Abdi Suleiman, Said musa, Yohana Nkomola kwa kuwataja wachache. 

February 08, 2018

WACHEZAJI WANAVUMILIA MENGI YA MASHABIKI ILA NYOSO KATUONYESHA MOYO WAKE.

NA. HONORIUS MPANGALA
Moyo umeundwa na nyama pamoja na mishipa mingi inayofanya kazi ya kusukuma damu Kwa pande zote.Ni moyo huu huu ambao wengi husema unawauma baada ya kuwasibu mambo ambayo hawata furahishwa nayo. Ni moyo pia ambao humfanya mtu akajisikia amani na furaha baada kuona moyo umeridhika na kufurahishwa na jambo fulani.

Katika Maisha ya kawaida kumekuwa na maneno chungu nzima yanayoweza kuhusisha moyo.Iko misemo kama 'Nina moyo wa nyama' pia imeibuka mingine ya kusema ' moyo sukuma damu sio vingine'. Yote hutokea kwasababu tunajua moyo ndo injini ndogo baada ya ubongo katika kuamua na kuatoa maamuzi ya kuchukizwa au kufurahishwa.Licha ya ubongo kudhibitiambo yote yanayomhusu binadamu lakini moyo niku cha aina yake katika mwili Wa bindamu.  
Tukio alilolifanya Juma Nyoso kwa shabiki wa Simba lina mafunzo pande zote mbili.

Upande Wa kwanza ni Kwa mashabiki Wa soka. Wanatakiwa kutambua wachezaji ni bindamu kama walivyo wao. Kila tendo afanyo mchezaji wakati mwingine hulifanya katika mazingira ya akili ya kawaida kama walivyo binadamu wengine. Ila itashi Wa mashibiki tumefikia hatua ya kuona wachezaji kama kitu Fulani chenye uhitaji tofauti na walivyo binadamu wengine.

January 18, 2018

KABWILI ASINGEKUBALI KUFUNGWA PENATI TANO ZA URA.

Na. HONORIUS MPANGALA
MIONGONI mwa utofauti ambao binadamu tunao ni jinsi ya kuzitumia akili zetu. Utofauti huo huweza kumtofautisha yule mwenye uwezo mkubwa katika kubaini jambo na kutafuta ufumbuzi na mwingine kubaini jambo kunachukua muda na kulifanyia ufumbuzi. Licha kuaminika kuwa tuko sawa lakini katika baadhinya nyanja hatuwezi kuwa sawa ndo maana wako warefu na wemgine wafupi ukiwalinganisha hao unapata utofauti. 

Yanga moja ya akili kubwa waliyoitumia kufanikisha saini ya Ramadhani Awam Kabwili Kwa mkataba Wa miaka mitano. Sijajua nani alisimamia kusaini Kwa Yohana Nkomola maana nilifikiri nae wangemalizana nae Kwa mtindo kama Wa Kabwili. Hata hivyo Kwa vile yuko katika milki yao wataweza kutenda jambo nae siku za usoni.


Licha ya mashaka makubwa wanayokuwa nayo mashabiki dhidi ya wachezaji vijana katika vikosi mbalimbali vya timu,ila hao ndio watu makini sana katika kitenda licha ya kwamba kuamua jambo kwao kunaweza kuwa na wasiwasi Wa hofu ya kuogoa kukosea. Wapo ambao wanakuzwa katika misingi ya kuamua Kwa kutenda Kwa wakati na kuamua Kwa ufasaha licha ya umri wao kuwa mdogo.

December 02, 2017

FURAHA YA MAZEMBE ILIYOPORWA UWANJA WA NDEGE NA KABILA

NA. HONORIUS MPANGALA 
Rais Joseph Kabila ni mmoja ya marais wa Afrika ambao ni wamashabiki wakubwa wa mchezo Wa soka. Amekuwa akisapoti sana mchezo Wa soka Kwa timu yao ya taifa inayoitwa chui. Wadau wengi wa soka wanakumbukumbu ambayo aliiweka kwa kuwapa zawadi ya magari kila mchezaji na viongozi wote walioshiriki katika michuano ya CHAN iliyofanyika mwaka Jana 2016 nchini Rwanda. 

 Kabila ameonekana mara nyingi sana katika viwanja vya michezo akihudhuria mechi mbalimbali.Hata katika video ya ule wimbo maarufu 'Leopards fimbu na fimbu' ulioimbwa na Felix Wazekwa umemwonyesha rais akikabidhiwa kombe la Chan mwaka 2009 na Nahodha Wa wakati huo Tresor Mputu,ambalo Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo walilichukua baada ya kuwafunga Ghana katika uwanja wa Felix Houpout-Boigny pale Abidjan Nchini Ivory Coast.

November 10, 2017

SOKA LA WACHINA, LIKABORESHWA UINGEREZA

NA.HONORIUS MPANGALA

INASADIKIKA Polisi wa China walikuwa wanacheza mchezo uliitwa 'Tsh-u' ikiwa na maana ya piga mpira. Mchezo huo ulipenyeza Japan na maeneo mengine ya Roma. 

Soka lilingia Uingereza mwaka 1066 wakati wa utawala wa Mfalme William. Kutokana na wachezajj wengi kupata matatizo ya vifo mfalme Edward na wengine kama Richard walipiga marufuku na kutoka kauli ambayo Kwa yoyote atakayehusika au kuonekana anacheza soka atenda jela.

November 03, 2017

RATIBA YA LIGI KUU TANZANIA BARA WIKI HII


October 27, 2017

WAAMUZI WA SOKA KATIKA JICHO LA JAMII.

NA HONORIUS MPANGALA
 
WAAMUZI wa soka wamekuwa wakitazamwa tofauti kulingana na wao wenyewe wanavyojiweka katika jamii ya wapenda soka. Wako ambao wameifanya fani hiyo kuwa moja ya vitu ambavyo vinaweza kuwapatia nafasi ya kucheza matangazo. Pia wapo ambao jamii imewachukulia tofauti kutokana na mitazamo yao.
Jonasia Rukyaa.
Kuna mitazamo hasi kwa baadhi ya wapenda soka waonapo waamuzi wa kike wakichezesha mchezo. Mitazamo hiyo inatokana na asili ya mchezo wenyewe unavyochukuliwa kama ni wa wanaume. Licha ya wanawake kuucheza lakini bado mitazamo hiyo imekuwa ngumu kuwatoka baadhi ya wapenda soka. Ndo maana hata wale wanawake wanaocheza soka ukiwatazama utafikiri wanaume Kwa baadhi yao.

Tanzania ina Mwamuzi wa kati maarufu Jonasia Rukyaa ambaye anafanya vizuri sana. Alikuwepo katika mashindano ya Afcon ya wanawake ikiyofanyika Kameruni. Pia baada ya kushiriki katika kliniki ya waamuzi Kule Ureno mwaka huu amekuwa na mwaliko 'appointment' ya uwepo katika kombe la dunia. Na yupo katika mshindano ya kombe la dunia la vijana wa chini ya miaka 17 Iliyofanyika India. 

October 17, 2017

UTAMU WA WIMBO WA TAIFA UKO KOMBE LA DUNIA.

NA. HONORIUS MPANGALA
 
ILIKUWA miaka Sita ya Ubabe wa soka barani Afrika kuanzia mwaka 2006 hadi 2012. Kila mpenzi wa soka alimfahamu Hassan Shehata,kila mpenzi wa soka alimfahamu Waile Gomaa. Ilikuwa nyakati za Misri kunyanyasa mataifa mengine ndani ya bara la Afrika. Ilimchukua Kameruni miaka tisa kulipiza manyanyaso aliyopata toka kwa Misri ya kiumeni mwaka 2008 pale Ghana.
Ni Misri ambayo iliipa hasara CAF kuunda kombe lingine la Afcon baada ya kulibeba lile awali Mara nne Mfululizo. Mwaka 2006 fainali zilizoandaliwa na Misri wakikutana na Ivory coast ya Didier Drogba.
KIKOSI CHA MISRI

Fainali ile iliisha kwa matuta na wenyeji kutwa taji. Licha ya kuwa na kikosi ambacho kilikuwa na vijana taklibani Saba wakitoka kikosi cha Al Ahly ambayo ilikuwa moto wa kuotea mbali. Hapa nawazungumzia Mohammed Barakat,Saeed Moward,Essam El Hadary,Ahmed Hassan,Hossam Hassan,Mohammad Mido,Mohammed Aboutrika na wengineo. Ilikuwa ni kikosi kilichojaa vipaji kikiwa na hamasa kubwa kutoka kwa kocha mzawa Hassan Shehata kiliwafanya wapinzani wafikirie Mara mbili zaidi.

October 14, 2017

WATU WASIOJULIKANA WATAIKIMBIZA AFCON U-17 2019

NA HONORIUS MPANGALA 
 
MWANDISHI maafuru wa fasihi kutoka Nigeria,marehemu Chinua Achebe katika kitabu cha 'Things Fall Apart' alisema kukimbia matatizo sio njia sahihi ya kutatua hayo matatizo. Wakati msomaji wa fasihi hiyo akiona kama burudani kusoma vibweka vya Okonkwo lakini kuna mafundisho katika kitabu kile. Nyakati zote huwezi kuona ugumu wa jambo kama halijakutokea.
Chinua ananifanya nihusianishe matukio ya watu wasiojulikana na hatima ya Nchi katika nafasi ya kuandaa fainali za mataifa ya Afrika kwa vijana wa chini ya miaka 17.
Serengeti Boys wakifurahia katika moja ya mabao waliyofunga katika mechi za kimataifa
Ukimya wetu katika kuchukulia kila jambo ni kitu kinachofanyika na tukashindwa kutambua tatizo au kuwabaini wahusika linaweza kutuondolea mwonekano wetu nje ya mipaka ya nchi.

Matatizo yanatakiwa kutatuliwa kwa kufahamu chanzo na kuchukua hatua ya kuyamaliza. Sisi kama Taifa tuna hamu kubwa na kuona tukifanikisha Michezo inafanyika vyema hapa nchini kwa kuhusisha sekta zote kushiriki vyema.
Labda nikumbushe jambo moja baada ya Afrika kusini kutangazwa kama waandaaji wa fainali za kombe la dunia mwaka 2010. 

October 11, 2017

CATALUNYA IMENIKUMBUSHA WIMBO WA TAIFA WA HISPANIA.

NA HONORIUS MPANGALA, 0628994409
 
ILIKUWA katika mechi ya kombe la dunia mwaka 2002,Korea kusini na Japan ndiko nilipohitimisha majibu ya maneno ya kusimuliwa. Kaka yangu alikuwa mtu aliyependa kunisimulia kuhusu vibweka vya kwenye soka tangu zamani na hajaacha hadi Leo. Naweza kusema ndiye aliyefanya nikawa napenda soka na kulichambua.
Wachezaji wa Hispania wakishangilia moja ya mabao waliyofunga.
Katika fainali zile pale Korea na Japan ndipo nilipoamini kweli taifa la Hispania halina maneno katika wimbo wake wa taifa. Ilikuwa katika moja ya mechi iliyokuwa na msisimko mkubwa kundi B, Hispania dhidi ya Afrika kusini. Mchezo uliopigwa katika uwanja wa Daejeon katika mji huo nchini Korea kusini.

October 02, 2017

NI VIGUMU KUREJESHA ZAMA ZA RTC NA RELI KIGOMA.

NA. HONORIUS MPANGALA
WENGI wanapajua kwa jina la utani mwisho wa reli. Ni kigoma mkoa wa kanda ya Magharibi ukiwa na sifa kemkem katika kila nyanja iwe medani ya siasa,sanaa na hata soka. Kabila la Waha ndio wenyeji wa mkoa huo lakini yako makabila mengine. Wako wabembe na wanyema pia. Moja ya nyimbo bora za bongo fleva 'Leka tutigite' wa Kigoma All stars ni kati alama ambayo inatumika kuutambulisha mkoa huo.Hifadhi ya Gombe na Mahale ambayo ina sokwe ni miongoni mwa kivutio , pia meli kongwe duniani iliyoundwa na wajerumani mwaka 1913 katika maandalizi ya Vita ya kwanza ya dunia MV Liemba iko Kigoma na ingali inafanya kazi hadi Leo.
Umati wa wapenda soka mkoa wa Kigoma wakitazama mechi ya fainali ya mashindano ya kugombea ng'ombe katika uwanja wa Lake Tanganyika.

September 22, 2017

USHAURI WA BURE KWA TFF

NA SAMWEL CHITANYA

MOJA kati ya nchi za Afrika ambazo raia wake wanapenda sana mchezo wa kandanda  duniani ni Tanzania. Watanzania wanaupenda sana mchezo Wa kabumbu. Ni mchezo unaopendwa na watu wengi duniani kote. Unaongoza kwa kupendwa.

Bahati mbaya sana pamoja na Watanzania kuupenda mchezo huu bado hawana mipango madhubuti ya kuufanya mchezo huu uwe wenye tija kwao. Mipango yao mingi ni yakucheza mpila na Siyo Mpira kama wenzetu wanavyo Fanya.

Timu yetu ya taifa huwa inashiriki katika kupigania nafasi ya kushiriki mashindano mbalimbali kama vile Kombe la dunia, kombe la mataifa Afrika na kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji Wa ligi za ndani.

Timu yetu hushiriki kikamilifu katika kuwania nafasi zote hizo. Tunajiamini kuwa Tuna timu bora ambayo inaweza kufanikiwa kufuzu mashindano yote hayo. Kujiamini siyo jambo baya lakini jitazame na uwezo wako kwanza.
Mara ya mwisho Tanzania kushiriki fainali za kombe la mataifa ya Afrika ilikuwa mwaka 1980. Miaka thelathini na saba(37) sasa imepita tangu tushiriki mashindano makubwa zaidi ya soka katika bara letu.
Kiungo mkabaji wa Taifa Stars, Himid Mao Mkami 

September 18, 2017

NYOTA YA SAMATTA

Bajaji ya shabiki wa Mbwana Samatta, ikiwa imeegeshwa katika mtaa wa Ijumaa, Sinza Kijiweni- Dar es salaam.

September 16, 2017

MIAKA 33, YANGA KASHINDA MARA MOJA UWANJA WA MAJIMAJI.

Na. Honorius Mpangala.
Labda kama ulikuwa hujui mpenzi wa soka la Tanzania. Toka mwaka 1984 hadi sasa mwaka 2017 klabu ya Yanga imepata ushindi katika uwanja wa Majimaji Mara 1 . Ni kaseke aliyeifunga Majimaji msimu uliopita goli moj.

Tangu zama za wachezaji waliopita klabu hiyo kama kina SHAIBU KAMBAGA,MBOPA LUOGA(NAHODHA) ,SELESTINE SIKINDE MBUNGA,MADARAKA SELEMANI,FRED MBUNA,ABDALLAH KIBADENI,PETER TINO, STEVEN MAPUNDA,ODO NOMBO,JUMA MPOLA (ZIZOU) na wengine wengi. Majimaji imefungwa Mara Moja.

Nyakati zote kwa miaka hiyo yanga aliambulia kipigo au sare ya magoli au isiyo ya magoli. Historia iko na inavunjwa pia lakini lazima vijana waendeleze kuweka ngumu kwasababu hatutaki mazoea.
                                                Bendera ya timu ya Majimaji

August 24, 2013

ZIARA YA MCHEZAJI WA ZAMANI WA MACHESTER UNITED, QUINTONE FORTUNE HAPA NCHINI KATIKA JUHUDI ZAKE ZA KUSAIDIA JAMII KAMA MWAKILISHI WA TIMU HIYO

FORTUNE na Mimi alipotembelea ofisini.

August 15, 2013

DRFA KUENDESHA SEMINA KLABU ZA LIGI KUU NA DARAJA LA KWANZA


Na Mwandishi Wetu, Dar es salaam
CHAMA Cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) kitaendesha semina ya siku moja kwa klabu 11 za Mkoa wa Dar es Salaa zinazoshiriki Ligi Kuu ya Vodacom na Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara ili kuboresha weledi na hatimaye kufanya vizuri.
Mada zitakazotolewa katika semina hiyo ni sheria 17 za mpira wa miguu, majukumu ya benchi la ufundi na jinsi ya utoaji habari kwa klabu.

Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa DRFA, Mohamed Mharizo semina hiyo imepangwa kufanyika Agosti  18 kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 11:00 jioni kwenye Uwanja wa Taifa.

Washiriki wa semina hiyo ni Mameneja wa timu, kocha, nahodha wa timu na Ofisa Habari kutoka katika klabu hizo.
Klabu hizo za Mkoa wa Dar es Salaam zitakazoshiriki semina hiyo ni Simba, Yanga, Azam FC, Ashanti United, African Lyon, Villa Squad, Trans Camp, Police Central, Green Worriors, Tesema na Friends Rangers.

Watoa mada katika semina hiyo watakuwa Mkurugenzi wa Ufundi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Sunday Kayuni, Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Waamuzi ya TFF, Omari Kasinde na Ofisa Habari wa TFF,  Boniface Wambura.

Mgeni rasmi katika semina hiyo anatarajiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadik.

KOCHA ARSENAL ATUA SONGEA



Na Amon Mtega, Songea

JOPO la makocha kutoka timu ya Arsenal  ya  Uingereza wamewasili Songea mkoani Ruvuma kwa ajili ya kutoa mafunzo ya ukocha ya siku tano ya mpira wa miguu kwa walimu wa shule 40.

Akizungumza jana na waandishi wa habari, Mratibu wa mafunzo hayo  Selwin Ngonyani  alisema makocha hao kutoka timu ya Arsenal  Uingereza wamefika mkoani hapa kutoa mafunzo kwa lengo la kuibua vipaji kwenye shule hizo.

Alisema mafunzo hayo yanafanyika kutokana na ushirikiano uliyopo kati ya Shule ya Sekondari ya wasichana ya Peramiho na Mtakatifu Arouse  ya Uingereza ambayo ina urafiki na timu ya Arsenal.
  
“Mafunzo hayo yatatusaidia kuwafundisha vijana wetu  shuleni  kwa kuibua vipaji vyao ili na sisi kwa siku za baadae tuwe na wachezaji wazuri wenye viwango vya hali ya juu,” alisema.

Kwa upande wake mmoja wa makocha hao, Tony David   alisema Tanzania ni nchi yenye vijana wenye vipaji vya michezo hasa mpira wa miguu kwa kuwa wanafundishika na kuelewa haraka.